Habari

Jumapili, 8 Februari 2026

ATHARI ZA KUTOWASHIRIKISHA WATU WENYE ULEMAVU KWENYE NGAZI ZA MAAMUZI

.NA, ASIA MWALIM NCHI nyingi hupanga mipango yake ya Kimaendeleo na kiuchumi kwa kuzingatia mambo mengi.Hii ni pamja na idadi ya watu wake na zaidi mahitaji yao, ikiwa pamoja na kuzingatia maumbile.
Katika hayo mazingatio limo kundi la watu wenye mahitaji maalum katika maisha yao ya kila siku na miongoni mwao ni wale wenye ulemavu. 
Takwimu za Umoja wa Mataifa zinaonesha takriban asilimia 15 ya watu duniani ambao ni zaidi ya bilioni moja ni wenye ulemavu, wengi wakiwa wanawake. Hata hivyo, kundi hili bado halijapewa umuhimu unaostahiki katika baadhi ya maeneo, hali inayowanyima haki zao za kikatiba na kidemokrasia.
 Miongoni mwa malalamiko yanayosikika hapa kwetu ni ya vyama vya siasa kushindwa kuwasimamisha watu wenye ulemavu majimboni na badala yake kutegemea nafasi za viti maalumu pekee. Wapo wanaouliza kama Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama.Samia Suluhu Hassan na Rais wa Zanzibar,Dk.Hussein Ali Mwinyi, wanawaingiza wanawake wenye ulemavu katika uteuzi wao kipi kinachofanya hali kama hiii kushindikana katika vyama vya siasa kuwaweka  kuwa wagombea katika uchaguzi? Matokeo ya sensa yanaonesha kiwango cha watu wenye ulemavu Tanzania kimeongezeka kutoka watu 93 katika mwaka 2012 hadi 112 mwaka 2022 kwa kila watu 1,000. 
Katika miaka ya karibuni Zanzibar imeshuhudia serikali ikiteua wanawake zaidi, wakiwemo wenye ulemavu katika nafasi za juu za uongozi. Katika mahojiano maalum wanawake wenye ulemavu walielezea wanavyotamani kuipata haki ya kuchaguliwa kwenye majimbo kwa njia nyepesi, kama ilivyo kwa watu wengine. Vyama vya siasa havijatoa umuhimu wa kusimaisha watu wenye ulemavu majimboni na hili limelezewa na wanwake wenye ulemavu kama ni ubaguzi.
 Jamila Borafya wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) alisema kundi hilo lina uwezo wa kuongoza nafasi za uwakilishi au ubunge majimboni na sio tu kupitia nafasi za viti maalumu. "Tunataka nafasi za majimboni na sio za viti maalumu pekee kwani tunao uwezo na uzoefu wa kutosha" alisema. Alisema ni vizuri wanawake wenye ulemavu wanapojitokeza kugombea wakapewa nafasi sawa na wagombea wengine na hata kuwapa kupaumbele.

Alisema mtindo wa sasa wa kutoa zaidi nafasi kwa wanaume sio sahihi na unahitaji marekebisho. 
Adil Mohammed Ally, Mratibu Jumuiya ya Wasioona Zanzibar (ZANAB), alisema watu wenye ulemavu wana himili kuongoza nafasi za majimbo, lakini ipo haja kwa vyama vya siasa kuzingatia hilo ile watu hao wapate haki yao ya kikatiba. Alishauri Tume ya uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) kuweka sheria madhubuti na msisitizo kwa vyama vya siasa kutoa kipaumbele kwa watu wa kundi hili watapotaka kugombea majimboni. Hata hivyo, aliwataka watu wenye ulemavu kujitokeza kwa wingi majimboni mwaka 2025 kwani jamii imebadilika na yamefanyika marekebisho ya mifumo ya kupiga kura kwa watu wenye ulemavu. Alitoa mfano wa katiba ya Zanzibar ya 1984, ambayo inaeleza katika kifungu 21(2) kila Mzanzibari anayo haki na uhuru wa kushiriki ukamilifu katika kufikia uamuzi wa mambo yanayomuhusu yeye na taifa. Vile vile katika marekebisho ya 2010 katiba imeeleza katika kifungu nambari 67 (1) kuwa kutakuwa na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wanawake kwa asilimia 40 ya wajumbe wakuchaguliwa katika majimbo. Aisha Ali Abdallah, kutoka ZANAB aliyeshiriki kugombea nafasi ya uongozi wilaya ya Chake chake, Pemba, alisema ushiriki wao katika kugombea nafasi za uongozi ni mzuri,lakini vyama vya siasa haviwapi nafasi. 
"Nilishiriki kugombea uwakilishi katika uchaguzi wa mwaka 2020, lakini sikuipata hiyo nafasi" alisema. Alisema hadi sasa Pemba hakuna kiongozi mwenye ulemavu ambaye wanaweza kumpa changamoto za kutatua matatizo yao kwa wakati. VIONGOZI WENYE ULEMAVU Mwantatu Mbarouk Khamis, Mwakilishi wa viti maalum kupitia Chama Cha Mapinduzi, (CCM) alisistiza haja ya wana siasa kuwaunga mkono watu wenye ulemavu kwa kuwapa nafasi majimboni ili waweze kushiriki katika vyombo vya maamuzi. Hadi kukamilika uchaguzi 2020, Katika Baraza la Wawakilishi kuna viongozi watatu tu waliopata nafasi hizo kupitia viti maalumu kwa tiketi za CCM. "Mwanamke mwenyewe ulemavu anao uchungu wa kusaidia jamii yake kupata maendeleo na hakuna sababu ya kuweka matabaka, Sote ni viumbe hatujakamilika, kila mtu ni mlemevu mtarajiwa" , aliongeza. VIONGOZI WA MAJIMBONI Mbunge wa Kiembesamaki, Mohammed Maulid, alisema jamii inapaswa kuwapa nafasi wanawake na watu wenye ulemavu kwani ni baraka na kuwakwamisha ni kutowatendea haki.Diwani wa Fukuchani, Fatma Ngwali Khamis, alisema licha ya hali yake na kukumbana na changamoto alishinda kupitia kura za wananchi kutokana na uwezo wake wa kuongoza na kuwataka watu wenye ulemavu kujitokeza zaidi majimboni licha ya magumu wanayopitia. Alisema wapo wanaodhani ukimuweka mtu mwenye ulemavu jimboni ni kama kupoteza nafasi, dhana iliyobebwa na jamii kubwa hasa wanasiasa. 
WANAHARAKATI 
Aliekua Mkurugenzi wa Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania TAMWA-ZNZ, Dk.Mzuri Issa, alisema licha ya jitihada zinazofanyika zipo changamoto wanazopata wanawake na watu wenye ulemavu kufikia malengo yao. Miongoni mwa changamoto ni baadhi ya viongozi wa dini, jamii na vyama vya siasa hawajaweka umuhimu kwa wanawake na watu wenye ulemavu kupewa nafasi za uongozi. Alisema wakati mwengine watu wenye ulemavu wanabezwa na kufanyiwa dhihaki kwa kuangaliwa hali zao na kipato chao na kuitaka jamii kubadilika. Alishauri sera na sheria za vyama vya siasa kusisitiza usawa kwenye nafasi za uongozi na maamuzi na kuvitaka vyombo vinavyohusika kusimamia haki. Vyombo hivi nipamoja na Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar (ZAECA) kuweka mustakabali mzuri kwa makundi yote.Ukhty Amina Salum, alisema sio sahihi kutumia dini kama kigezo cha kumzuia mwanamke kuongoza, kwani dini inatambua uwezo wa mwanamke kuongoza. Bi Asha Abdi, Mwenyekiti wa Mtandao wa Jinsia Zanzibar, alisema kuna umuhimu wadau na wanaharakati kulifanyia kazi sula la watu wenye ulemavu, hasa wanaogombea uongozi. TUME YA UCHAGUZI YA ZANZIBAR (ZEC) Mkurugenzi wa Uchaguzi Zanzibar, (ZEC)Thabit Idarous Faina, alisema kazi ya tume ni kupokea maombi ya wagombea waliopitia mchakato katika vyama vyao. Lakini ili kuondosha upendeleo usio wa lazima ni vizuri kwa vyama vya siasa kuliangalia hili kjwa undani ili kuondoa tataizo liliojitokeza.
 Alisema tatizo la usimamizi wa wagombea ni kwa vyama kutowasilisha majina ya agombea mapema ili kuhakikisha asilimia 40 ya wanawake wagombea inafikiwa. Alisema katika kueleka uchagyzi wa 2025, ZEC itaendelea kushirkiana na vyama vya siasa ili kupambana na rushwa na kuhakikisha wanawake wanapewa kipaumbele ili waweze kushiriki kwa asilimia kubwa zaidi. Kwa hali ilivuo sasa suala la vikwazo ambavyo wanawake na watu wenye ulemavu wanapambana navyo wanapoamua kugombea nafasi za uongozi ni tatizo inalohitaji kufanyiwa kazi ya ziada.
 IDARA YA WATU WENYE ULEMAVUKatibu Mtendaji wa Baraza La Taifa la Watu wenye ulemavu Zanzibar, Ussy Khamis Debe, alisema ni vyema Tume ya uchaguzi na mabaraza ya vyama vya siasa kuweka mazingira rafiki ya watu hao kupata nafasi hizo.Aliitaka jamii na vyama vya siasa kuacha kuwatenga na kutokana na dhana potofu zinazotumika kuwazuwia wanawake na watu wenye ulemavu wasigombee uongozi. 
JUMUIYA YA WANAWAKE WENYE ULEMAVU ZANZIBAR (JUWAUZA) Mkurugenzi Mtendaji Jumuiya ya Wanawake Wenye Ulemavu Zanzibar, Bakar Omar Hamad, alieleza kuwa watu wenye ulemavu na hasa wanawake wanapitia wakati mgumu wanapotamani kuwa viongozi. Katika mwaka 2020 kupitia vyama vya siasa takriban watu wenye ulemavu 30 walijitokeza kugombea nafasi tofauti majimboni na mwanamke mmoja mwenye ulemavu alishinda nafasi ya udiwani kati ya majimbo yote 50 ya Unguja na Pemba. Mwenyekiti wa Baraza la Watu Wenye Ulemavu, Salma Haji Saadat, alisema vyama vya siasa vinao wajibu wa kuhakikisha watu wenye ulemavu wanapewa kipaumbele katika nafasi za uongozi.
 Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Zanzibar, Abeda Rashid alisema licha ya changamoto zinazowagusa wanawake, lakini wamenufaika na fursa fursa hizo katika miaka ya karibuni.Abeda alisema kuna nafasi muhimu katika taasisi za serikali zinazoshikiliwa na wanawake. Miongoni mwao ni ya yeye amabye ni mwenye ulemavu kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii. Aliwapongeza wadau maendeleo na taasisi mbali mbali ikiwemo WILDAF, TAMWA, JUWAUZA, kwa kuwa mstari wa mbele kuwashirikisha wanawake kwenye mafunzo ya kuwezesha kushika nafasi za uongozi.
 MATAMKO MBALIMBALI YALIOLENGA USAWA Dira ya maendeleo ya Zanzibar ya mwaka 2050 imekusudia kuongezeka kwa fursa kwa makundi ya watu wasiojiweza wakiwemo watu wenye ulemavu, wanawake watoto na wazee. Itifaki ya Jumuiya ya Maendeleo ya nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) mkataba wake wa kikanda uliotiwa saini mwaka 2008 na nchi wanachama wake ikiwemo Tanzania, wenye vifungu 43 unaelekeza nchi hizo kuzingatia suala la haki na usawa kati ya wanaume na wanawake katika suala la uongozi. Kwa muhtasari ipo haja ya kulifanyia tathmini suala hili ili kuhakikisha watu wenye ulemavu na hasa akina mama wanatendewa haki na jamii yetu. Kwa muda mrefu na hadi sasa umepatikana uthibitisho wa kutosa wa kuonyesha uwezo wa watu wneye ulemavu, wanaume na wanawake, kushika hatamu na kuwa viongozi wa kupigiwa mfano.Moja ya njia ya kuliondoa tatizo hili ni kuongeza idadi yao kupitiamajimbo kwani hii itasaidia kupaza sauti zao kwenye vyombo vya maamuzi, hasa wakati wa kutungwa sera mbali mbali. 
Mwisho

Jumanne, 3 Februari 2026

MAENDELEO YA YA ELIMU YA MAANDALIZI NDANI YA MIAKA 62 YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR YAKUPIGIWA MFANO,,NEEMA KWA WOTE BILA UBAGUZI

 AMINA AHMED  MOHD

  JEE !  WAJUWA KABLA      Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964, elimu ya maandalizi  ndani ya visiwa vya unguja na Pemba  haikuwa rasmi, na nathubutu kusema haikuwepo kabisa ! hukukatika maeneo iliyokuwepo  ilitolewa kwa upendeleo wa kijamii na kikabila, na watoto wengi wa tabaka la chini watoto wa mskini, wakwezi na wakulima  hawakupata nafasi ya kujiunga na skuli za maandalizi ,huku Elimu ikibaki kuwa ya kikundi kidogo cha watotokutoka familia za wenye uwezo  na si haki ya kila mtoto.Yote hayo sababu kubwa ilikuwa Mfumo wa elimu ulikuwa ni wa kikoloni na wakisultani, ukilenga zaidi watoto wa tabaka la juu mijini, huku vijijini kukikosekana kabisa huduma za elimu ya awali ambayo kwa sasa inatambulika kama elimu ya maandalizi .HISTORIA YA ELIMU YA MAANDALIZI ZANZIBAR KABLA YA MAPINDUZI  YA ZANZIBAR YA MWAKA 64  UPATIKANAJI WA ELIMUElimu ya maandalizi haikuwa sehemu ya sera ya serikali ya kisultani. Hakukuwa na mtandao wa  skuli  za serikali kwa watoto wote; badala yake  skuli nyingi zilikuwa za binafsi na nyentine zikiwa  kidini.Elimu ya awali haikujulikana kwa kiwango cha kitaifa, bali ilikuwa ni ya kikundi kidogo cha watu wenye uwezo na maeneo yaliyokuwa rafiki kufikika maeneo ya unguja mjiniWatoto wachache wa tabaka la juu, hasa wa asili ya Kiarabu na kiswahili wa mjini, ndio waliopata nafasi ya kujiunga na skuli za awali,huku Vijijini, watoto walitegemea madrasa na elimu ya dini kama njia pekee ya skuli za maandaliz katika kujifunza .Mfumo wa elimu ulikuwa wa kikoloni na kisultani, ukilenga zaidi watoto wa tabaka la juu.Skuli  chache zilikuwepo, nyingi zikiwa mijini na hazikuwafikia watoto wa vijijini.Elimu ya maandalizi haikuwa rasmi, watoto wengi walijifunza kupitia madrasa au elimu ya jadi.Uwiano wa walimu kwa wanafunzi ulikuwa duni, walimu wachache na wengi wakiwa wageni.Huduma za kijamii skulini  hazikuwepo, hakuna lishe shuleni wala ruzuku kwa wanafunzi.Uandikishaji ulikuwa mdogo sana, idadi kubwa ya watoto wa Zanzibar hawakupata nafasi ya kusoma elimu ya maandalizi . Walimu wachache walikuwepo, wengi wakiwa wageni au wa tabaka la juu.Idadi ya watoto waliopata elimu ya maandalizi ilikuwa ndogo sana, ikilinganishwa na idadi ya watoto wa Zanzibar.Hakukuwa na mafunzo maalum ya ualimu wa maandalizi; walimu walitegemea uzoefu wa madrasa au elimu ya msingi ya kikoloniELIMU BAADA YA MAPINDUZI  1964–  ILIPOFIKIA MIAKA 62   MWAKA HUU 2026)Kuna mageuzi makubwa  mabadiliko na maendeleo ya elimu  yamefikiwa  miongoni mwa hayo ni pamoja na Elimu sasakuwa  haki ya kila mtoto,kwa lazima  bila ubaguzi wa kijamii,dini siasa wala  uchumi . Kabla ya Mapinduzi ya mwaka 1964, elimu ya maandalizi Zanzibar haikuwa rasmi, haikuwa jumuishi, na iliwafikia wachache tu wa tabaka la juu mijini. Mapinduzi ya Zanzibar yalibadilisha hali hii kwa kuifanya elimu kuwa haki ya kila mtoto bila ubaguzi, na kuanzisha mtandao wa shule za maandalizi na msingi unaofadhiliwa na serikali. Skuli zimeongezeka kwa kasi ndani ya miaka 62 ya Mapinduzi  ya mwaka 1964  Kwa sasa kuna zaidi ya 262 za maandalizi  zinazopata ruzuku ya Serikalikatka kutoa huduma bora kwa wananchi za serikali na binafsi ..Ndani ya miaka 62 ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar kuna Ukarabati na ujenzi mpya: Skuli 97 za maandalizi zinazojumuisha na a msingi zinaendelea kukarabatiwa, na ujenzi wa shule mpya 36 (21 za maandalizi, 15 za msingi)ukiendelea katika maeneo mbali mbali Unguja na Pemba.Ongezeko la Walimu wapya,889 wamepangiwa kazi  mwaka 2025/26  pekee, wakisaidia kupunguza uwiano wa walimu kwa wanafunzi jambo ambalo kabla ya miaka 62 ya mapinduzi ya  ya 1964 hayakuwepo .Kuna ongezeko la Uandikishaji wa Wanafunzi , Wanafunzi 105,101 sawa na asilimia  (82.5%) wameandikishwa katika skuli  maandalizi maeneo yote  Unguja na Pemba hadi kufikia miaka 62 ya mapinduzi matukufu ya Zanzibar yalioasisiwa na  Hayat mzee Abeid Aman Karume .Ambapo huduma  za lishe Maskulini kabla ya miaka  ya Miaka 62 ya Mapinduzi ya Mwaka 1964 hazikuwepo kabisa lakini kwa  ndani ya miaka 62 ya Mapinduzi hayo Matukufu   huduma za lishe zimeongezeka na kufikia asilimia  50  na wanafunzi    wapatao 63,099 .hupata lishe bora kupitia ruzuku ya serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.  Sekta ya elimu ya maandalizi na msingi Zanzibar imepiga hatua kubwa baada ya Mapinduzi ya mwaka 1964, ikilinganishwa na hali ya elimu kabla ya Mapinduzi. Leo, miaka 62 ya Mapinduzi hayo  hku idadi ya mageuzi na mabadiliko katika upatikanaji wa Haki hiyo  zikionesha  kuongezeka kupatikana huduma  bora za elimu ya maandalizi  kwa uandikashaji wa wanafunzi bila ubaguzi wa aina yeyote, Lishe, elimu bora, waalimu , majengo  bora ya kupata elimu Mapinduzi yam waka 1964 hadi kufika kilele cha miaka 62 mwaka huu 2026 january 12  kumekuwa na mageuzi makubwa katika elimu ya maandalizi na msingi kutoka mfumo wa kikiloni uliokuwa wa kibaguzi na wenye  upatikanaji mdogo wa utoaji elimu  ufinyu wa maeneo ,lishe ,uwandikishaji duni na matabaka wa waalimu wachache mitaala isyorasmi hadi sasa  kuwa kasi ya mageuzi  kutoka kadhia hizo na kuwa  Zanzibar ya miaka 62 ya mapinduzi yenye  mfumo mjumuishi wa elimu ,takwimu thabiti za uandikishaji zenye kuangalia hali za wananchi,waalimu  bora, miundombinu bora  huduma za kijamii  skulini   yote hayo ni mafanikio  ya miaka 62 y MapinduizI ya Zanzibar   katika kuinua maisha ya wananchi kupitia elimu bora ambayo ndio ufunguo wa mafanikio ya taifa na mtu mmoja mmoja baadae

Jumamosi, 31 Januari 2026

BINAADAMU NA MCHANGO WA MABADILIKO YA TABIANCHI.


Na,TIME KHAMIS PEMBA.
  Binaadamu wana mchango mkubwa katika mabadiliko ya tabianchi, hasa kupitia shughuli zao za kila siku. Mabadiliko ya tabianchi yanamaanisha mabadiliko ya muda mrefu katika hali ya hewa kama ongezeko la joto duniani, mabadiliko ya mvua, na matukio ya hali ya hewa ikiwemo jua kali. 
Jinsi binaadamu wanavyochangia Matumizi ya nishati ya mafutakuchoma makaa ya mawe, mafuta ya petroli na gesi asilia (kwa usafiri, viwanda, na umeme) hutoa gesi chafuzi kama  kobondiaxyde  (CO₂) ambazo zinaongeza joto duniani. 
Ukataji wa misitu unofanywa na Binaadamu huchangia kwa kiasi kikubwa mabadiliko hayo kwani kuwepo kwa misitu husaidia kunyonya CO₂, na  inapokatwa, uwezo huo hupungua na gesi chafu  huongezeka. Kwenye shughuli za Kilimo na ufugaji baadhi ya mbinu za kilimo na ufugaji hutoa gesi kama methani (CH₄), hasa kutoka kwa mifugo ambayo nayo huchangia kupatikana na mabadiliko tabia nchi kama gesi hiyo haikuwa na udhibiti. Aidha Uzalishaji wa taka taka  ovyo zikioza bila kudhibitiwa hutoa gesi chafuzi na Athari za mabadiliko ya tabianchi huongezeka kwa joto na ukame ,mafuriko na mvua zisizotabirika,kupungua kwa uzalishaji wa chakula,Athari kwa afya ya binadamu na viumbe hai               SULUHISHO NA HATUA ZA KUCHUKUA Kutumia nishati mbadala (jua, upepo, maji),kupanda miti na kulinda misitu, kuboresha mbinu za kilimo endelevu,kupunguza taka na kusindika upya (recycling),kuelimisha jamii na kuhimiza sera rafiki kwa mazingira kwa kifupi, binaadamu ni sehemu ya tatizo lakini pia wanaweza kuwa sehemu ya suluhisho kwa kuchukua hatua zinazolinda mazingira.       
   MOJA YA MBINU ZA KUZUWIA ATHARI HIYO Mradi ZanADAPT
 ni mpango wa utekelezaji unaolenga kusaidia jamii za Zanzibar kupambana na athari za mabadiliko ya tabia nchi kwa njia ya kujenga ustahimilivu wa mazingira, kijamii na kiuchumi, hasa kwa wanawake na familia zao.                
       MRADI  HUO  UNAVYOSAIDIA: 
 Kujenga ustahimilivu wa mazingira kupitia njia za asili na za mitaaMradi unatumia mbinu za nature-based adaptation (urejesho wa mazingira), kama vile: Kulinda na kurejesha misitu ya mikoko, ambayo husaidia kupunguza athari za hali ya hewa kama mafuriko, kuzuia ukame, na kuhifadhi vyanzo vya uhai pwani.  
Misitu ya mikoko pia huingiza gesi chafu kama dioksidi ya kaboni, hivyo kuchangia kupunguza mabadiliko ya tabia nchi.  Kilimo mseto na kilimo chenye ustahimilivu wa hali ya hewa, ambacho hutoa chakula na kipato kwa wakazi huku kinapambana na athari za mabadiliko ya tabia nchi. 
 Kuendeleza mazao na mbinu za kilimo rafiki kwa mazingira ili kuimarisha ardhi na kuongeza ustawi wa ardhi kwa wakati wa mvua nyingi au ukame.        
  MBINU NYENGINE ZINAZOTUMIWA NA MRADI.  
  Uwezeshaji wa wanawake na utekelezaji wa kijamii ,moja ya malengo makuu ya mradi ni kuongeza ushiriki na uongozi wanawake katika shughuli za kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi, Kuwawezesha wanawake kupata ujuzi na nafasi za uongozi kwenye juhudi za kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na usimamizi wa rasilimali. 
 Kuunda vikundi vya wanawake wanaojifunza na kushirikiana kuhusu mbinu za kilimo, uhifadhi wa misitu, na maamuzi ya utunzaji wa ardhi.  
Kupitia mradi, wanawake wengi wameweza kushika nafasi za uongozi ndani ya vikundi vya wakulima na utekelezaji wa shughuli za mazingira.   Kujenga uwezo na elimu kuhusu mabadiliko ya tabia nchiZanADAPT inajenga uwezo kwa kutowa mafunzo kwa wadau. Mafunzo na uhamasishaji wa wakazi kuhusu mabadiliko ya tabia nchi, jinsi ya kuyakabili, na umuhimu wa kutunza mazingira kwa ustawi wa maisha yao.  Kupitia vikundi vya wakulima, wadau hupata ujuzi wa mbinu rafiki za kilimo na usimamizi wa maliasili.  
Mradi pia unalenga kuboresha ufahamu wa kijamii juu ya usawa wa kijinsia na nafasi za wanawake katika juhudi za kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.            USHAHIDI WA HILO  MRADI 
wa usawa wa kijinsia, utunzaji wa mazingira na ustawi wa kijamii na kiuchumi ‘Zanz Adapt’ umewapa mafunzo ya ujasiriamali wa kusarifu bidhaa mashambani wanawake wa shehia zilizofikiwa na mradi huo. Shehia hizo ni  Chwale, Kiuyu, Mchangamdogo na Kambini Wilaya ya Wete ambapo mafunzo yaliyotolewa ni pamoja na upikaji wa sambaro la embe, chai masala, utengenezaji wa makwaru ya ndizi na pilau masala ambazo zinatokana na mazao yanayolimwa kupitia kilimo msitu. 
Anazungumza na Mwandishi wa Makala hii Afisa kilimo msitu  na usawa wa kijinsia  kutoka taasisi ya CFP Sada Juma Segeja amesema hatua hiyo ni miongoni mwa kuwawezesha wanawake wa vijijini  kufikia fursa mbalimbali za kiuchumi na kujipatia kipato. Analifahamisha lengo la kufanya mafunzo hayo  ni kuongeza thamani  ya zao la ndizi, maembe kwa kufanya achari, viungo (spices) ambayo ni katika mazao yanayolimwa katika kilimo msitu  na kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.“Katika kufanya harakati hizi za ujasiriamali zitasaidia kukata miti ya mikandaa kwa shughuli za kujipatia kipato, yanayochangia maji kupanda juu , kuuwa mazalio ya samaki na kukosekana kwa mvua na kusababisha mabadiliko ya tabia nchi”alisema.
JEE NAO WASHIRIKI WA MAFUNZO WANASEMAJE
Washiriki wa mafunzo hayo Maryam Mbarouk  Khamis na Subeha  Suleiman Sultan walisema mafunzo hayo yatawakomboa  kiuchumi na kimaisha huk  wakivitaka vyombo vya habari kuhakikisha wanazisemea changamoto zao zinazorejesha nyuma maendeleo ya maisha yao. Mafunzo hayo ya usarifu wa mazao ni miongoni mwa utekelezaji wa mradi wa usawa wa kijinsia, utunzaji wa mazingira na ustawi wa kijamii na kiuchumi Zanz Adapt unaotekelezwa Chama cha waandishi wa habari TAMWA, wanawake Zanzibar CFI na jumuiya ya misitu  ya jamii Pemba CFP kwa ufadhili wa serikali ya Canada.     
MATOKEO YA MRADI HADI SASA 
Kwa mfano, matokeo yaliyorekodiwa (kabla ya 2025) ni pamoja na Kuunga mkono wanawake wasiopunguwa  14000  (hasa wanawake) katika kufanya kazi za kulinda mikoko, kuanzisha kilimo cha mseto, na usimamizi endelevu wa ardhi.  Kuunda vikwazo vya mafunzo vya wakulima kwa mazoea ya hali ya hewa,kushiriki wanawake zaidi katika maamuzi ya kijamii na mazingira ndani ya jamii .
Mradi ZanADAPT unasaidia kupambana na mabadiliko ya tabia nchi kwa kuhifadhi na kurejesha misitu ya mikoko kwa ustawi wa mazingira, kuendeleza kilimo chenye ustahimilivu wa hali ya hewa.    Kukuza ujuzi na uwezo wa jamii kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi, kuinua wanawake kiuchumi na kijamii katika juhudi za kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa.             
         MKUFUNZI KUTOKA MRADI WA ZAN ADAPT .
 Ofisa kutoka mradi wa ZanAdapt Meiya  Mbarouk Mussa alisema endapo wanawake   watajishughulisha na ujasiriamali wataweza kujikomboa katika hali duni na kuweza kuongeza kipato kitakachowakimu katika maisha yao.“Niwaombe munapotayarisha bidhaa zenu kufuata sheria ikiwemo ya usafi binafsi na eneo husika, usalama na uhakika wa munachokizalisha kufanya hivyo mutapata mafanikio na mutajiwezesha zaidi”, alisema.Aidha kwa vile Binaadamu mwenyewe ameshafahamu juu ya uharibifu anaofanya unavyomuathiri kimazingira wameanza kuchukuwa juhudi ya kuhifadhi mazingira kwa kukabiliana na tabia nchi .Kikundi cha Uhifadhi wa Mazingira katika kiji cha Shengejuu mkoa wa Kaskazini Pemba kimeamuwa kupanda miti ya mikoko ipatayo elfu kumi kwa ajili ya kukabiliana na mabadiliko tabia nchi.             
    JAMII NA TAASISI ZA KIMAZINGIRA.
Katibu wa kikundi hicho Hamad Omar Salim akizungumza na Makala hii anasema wameamuwa kufanya hivyo baada ya kuona mashamba ambayo walikuwa wanayatumia kwa kilimo cha Mpunga huko katika eneo la Ambasha Shengejuu kuvamiwa na maji ya Chumvi na hivyo kuwakosesha wananchi kupata eneo la Kilimo.‘’ Mwanzo eneo hili wazazi wetu walilitumia kwa kilimo lakini baada ya wanaadamu wenyewe kuliathiri kwa kukata miti , ya mikoko na majani mengine makubwa yaliokuwa yanahifadhi maji yasipande juu tumekuwa na athari kubwa sana’’, anasema.Katibu wa jumuiya ya uhifadhi wa mazingira ( JIKEUMA) Kisiwa panza wilaya ya Mkoani Pemba Juma Ali Mati wakati anazungumza na mwandishi wa Makala hii anasema ene la Kisiwa panza limeathirika sana na mabadiliko tabia nchi kutokana na matumizi mabaya yanayofanywa na binaadamu mwenyewe ikiwemo kukata mikoko na kuchukuwa mchanga sambamba na Sunami iliathiri maeneo mengi ya Kisiwa cha Pemba. Anaeleza kuwa kutokana na athari hizo za mabadiliko tabia nchi jumla ya familia 100 zimekosa sehemu za kilimo na hivyo walitumia shilingi milion 500 ambazo walipatiwa kupitia mfuko wa kusaidia nchi maskini.Hata hivyo anasema fedha hizo zilitumika kwa kupunguza uharibifu wa maeneo yalioathiriwa na mabadiliko tabia nchi lakini sio kuondosha tatizo hilo , hivyo Binaadamu anawajibu wa kuhakikisha anapambana kwa kila hali ili kudhibiti mabadiliko hayo.                             MWISHO.

Alhamisi, 8 Januari 2026

DINI HUFUNDISHA KUWA WANAUME NA WANAWAKE NI SAWA, WANAWAKE WANAPASWA KUHESHIMIWA, NA HAKI ZAO ZA KURITHI MALI LAZIMA ZIPEWE KWA HAKI NA UADILIFU

Na ,Time Khamis
  PEMBA.
DINI NDIO  mfumo wa maisha ya kila siku ya mwanadamu ambapo imekuwa muhimili wa maisha ya binadamu kwa karne nyingi, ukitoa  mwongozo wa maadili, sheria, na taratibu za kijamii, moja ya hoja zinazojitokeza mara kwa mara ni kutambuliwa  nafasi ya dini katika kuimarisha au kudhoofisha usawa wa kijinsia kwa kupotoshwa maana dhamira na malengo ya maelekezo ya dini kutoka kwa baadhi ya watu.
 Wanawake, kwa muda mrefu, wamekuwa wakikabiliwa na changamoto za kijamii na kiuchumi, hususan katika suala la urithi wa mali,  Makala hii inalenga kuchambua kwa kina namna mafundisho ya dini yanavyoweza kuunga mkono usawa wa kijinsia, kulinda haki za wanawake, na kuondoa tafsiri potofu zinazowanyima nafasi katika urithi na kupelekea kukosa fursa mbali mbali za kujiendeleza .
Mafundisho ya Dini Na Msingi wa MaadiliMafundisho ya dini yanajengwa juu ya misingi ya imani na maadili yanayolenga kuongoza maisha ya waumini.
 Dini nyingi, ikiwemo Uislamu, Ukristo, na dini za jadi za Kiafrika, zinahimiza heshima, uadilifu, na upendo. 
Hata hivyo, tafsiri za maandiko ya kidini mara nyingi zimekuwa zikiegemea katika mila na desturi za kijamii, na hivyo kuathiri namna haki za wanawake zinavyotekelezwa.
 Ni muhimu kutambua kuwa msingi wa dini nyingi ni kuhimiza usawa na heshima kwa kila binadamu, bila kujali jinsia.Usawa wa Kijinsia na DiniUsawa wa kijinsia ni dhana inayohusu kutoa nafasi sawa kwa wanaume na wanawake katika nyanja zote za maisha, elimu, ajira, uongozi, na familia. Mafundisho ya dini yanapochukuliwa kwa tafsiri ya kina, yanaweza kuwa chachu ya kuimarisha usawa huu ,Uislamu, Qur’an inatambua haki za wanawake katika urithi na mali huku Ukristo nao  kupitia  Injili unasisitiza upendo na usawa wa binadamu wote mbele za Mungu,bila kuzisahau Dini za jadi, Zinazohimiza mshikamano wa kijamii na heshima kwa kila mwanajamii bila kujali jinsia yake . Hivyo, dini si kikwazo cha usawa wa kijinsia, bali tafsiri potofu ndizo zinazozua changamoto.Heshima kwa Haki za WanawakeWanawake mara nyingi wamekuwa wakipuuziwa katika masuala ya kijamii na kifamilia. 
Mafundisho ya dini yanaposisitiza heshima na uadilifu, yanatoa nafasi ya kutambua na kulinda haki za wanawake,kama vile ,Wanawake kuwa na haki ya kurithi mali ya familia,Wanawake Kuwa na haki ya kushiriki katika maamuzi ya kifamilia na kijamii,Wanawake Kustahili heshima sawa na wanaume katika nafasi za kiroho na kijamii.
Inathibitisha kuwa Dini ndio , chombo cha kuimarisha heshima na haki za wanawake.Urithi na Nafasi ya WanawakeSuala la urithi ndio ambalo  limekuwa moja ya changamoto kubwa katika kulinda usawa wa kijinsia. Katika jamii nyingi, mila na desturi zimewanyima wanawake haki ya kurithi mali ya familia. Hata hivyo, maandiko ya kidini yanaonyesha wazi kuwa wanawake wana haki ya urithi.
Dini ya Uislamu, ndani ya Qur’an (Surah An-Nisa) inasema wanawake wana sehemu ya urithi, ingawa mara nyingi tafsiri za kijamii zimepunguza nafasi hiyo.Huku katika dini ya Ukristo nayo  Mafundisho ya upendo na usawa vinaweza kutumika kuhimiza heshima kwa haki za wanawake katika urithi.
Huku tatizo linabaki kuwa  si mafundisho ya dini yenyewe,ndiyo yanayomnyima fursa mwanamke  bali tafsiri na utekelezaji wake katika jamii ndio kikwazo  kinachoendelea kuwakwamisha kimaendeleo Kwanini tafsiri za maandiko na mafundisho ya dini  ni kikwazo Moja ya changamoto kubwa ni tafsiri zinazotolewa na viongozi wa dini na jamii. 
Mara nyingi tafsiri hizi zimeegemea zaidi katika mila na desturi za kijamii kuliko maandiko ya kidini yanavyoelekeza husuan ni katika jamii hapa kisiwani Pemba , Hii imepelekea wanawake kupuuzwa katika masuala ya urithi na haki nyingine,sababu kuu  nilizozibaini wakati wa kuandaa uchambuzi huu zikiwa ni pamoja na ,Tafsiri potofu zinawanyima wanawake nafasi ya kurithi,Mila kandamizi zinapingana na misingi ya dini,Uelewa mdogo wa maandiko ya kidini unachangia ukosefu wa usawa.
Viongozi wa DiniViongozi wa dini wana jukumu kubwa katika kuhimiza usawa wa kijinsia, Kwa kutumia mafundisho ya dini, wanaweza kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa kuheshimu haki za wanawake,Wanaweza kupinga tafsiri potofu zinazowanyima wanawake haki,Wanajukumu la kuhimiza tafsiri mpya zinazolenga usawa lakini pia Wanaweza kushirikiana na serikali na jamii kuimarisha haki za wanawake.
Jamii Jamii pia ina jukumu kubwa katika kuimarisha usawa wa kijinsia.
 Kwa kuzingatia mafundisho ya dini yanayohimiza heshima na haki, jamii inaweza kubadilisha mitazamo na desturi zinazowanyima wanawake haki zao,Jamii inaweza kuhimiza elimu kwa wanawake,Jamii inaweza kupinga mila kandamizi,Jamii inaweza kushirikiana na viongozi wa dini na serikali kulinda haki za wanawake.Mafundisho ya dini yanayounga mkono usawa wa kijinsia ni chachu ya mabadiliko ya kijamii. 
Kwa kusisitiza heshima kwa haki za wanawake katika urithi, dini inaweza kuwa nyenzo ya kuimarisha usawa na haki katika jamii.
 Changamoto kubwa ni tafsiri potofu na utekelezaji usiozingatia misingi ya dini. Hivyo basi, kuna haja ya kufanya tafsiri mpya na kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa usawa wa kijinsia.Ikumbukwe kuwa Usawa wa kijinsia si suala la kisiasa pekee, bali ni suala la kiimani na kimaadili. 
Mafundisho ya dini yanaposisitiza heshima na haki, yanatoa nafasi ya kuhakikisha kuwa wanawake wanapata nafasi sawa katika urithi na nyanja nyingine za maisha. Hii ni hatua muhimu katika kujenga jamii yenye haki, usawa, na maendeleo endelevu.

Jumanne, 6 Januari 2026

MRADI WA ZANZ ADAPT ,WAMUIBUA SEMENI KUWA MFANO WA UONGOZI,KATIKA KUPIGANIA MAZINGIRA DHIDI YA ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIA YA NCHI,AUNGWA MKONO NA WENGINE

Na, TIME KHAMIS 
  KATIKA  kijiji cha Mchanga Mdogo, Wilaya ya Wete, Mkoa wa Kaskazini Pemba, jina la Semeni Suleiman Hamad limekuwa mfano wa kuigwa hasa kwa wenye kiu ya kupata maendelkeo kupitia shughuli zao za kila siku kijijini humo Mwanamke huyu mwenye umri wa miaka 39 amebadili mwelekeo wa maisha yake kutoka jitihada za kujikomboa kiuchumi binafsi,na kimazoea  na sasa amejikita katika mapambano ya kulinda mazingira dhidi ya athari za mabadiliko ya tabianchi,huku lengo lake kubwa likiwa ni kujikomboa na umasikini wa kipato kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi yasiwe kikwazo cha kurudisha nyuma jitihada zake za kujikomboa kiuchumi.
 Kupitia juhudi zake, jamii yake wakiwemo akina mama wameanza kumuunga mkono huku wakiwa na matumaini  mpya na mshikamano wa kijamii katika kupanda Kandaa, kulinda kuhifadhi na kuitunza ili isiwaletee athari Safari ya Semeni ilianza kupitia mafunzo yaliyobadilisha mwelekeo wake ,yaliotokana na  mradi wa Zanzibar Women Leadership Climate Change and Adaptation  Zanz Adapt), mradi unaotekelezwa na Jumuiya ya Uhifadhi wa Misitu Pemba (CFP) kwa kushirikiana na Jumuiya ya Uhifadhi wa Misitu Kimataifa (CFI), pamoja na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA ZNZ), kwa ufadhili wa Canada Global Affairs.

Mradi huo wa  ZANZ ADAPT ambao lengo lake kuu ni kumsaidia mwanamke  katika maswala ya kuongeza kipato  kwa  kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi kupitia shughuli zao za  kiuchumi ikiwemo kilimo  msitu, mboga na matunda,  mikoko , pamoja na kuongeza usawa wa kijinsia   katika uongozi.Kwa vile yote hayo katika baadhi ya maeneo yamekuwa  yanafanyika kimazoea bila utaalamu huku waathirika wakubwa wakiwa ni  wanawake ,  na baadhi ya maeneo yakiwa ni miongoni mwa  maeneo yalioathoriwa na mabadiliko ya tabia ya nchi juhudi za kuwasaidia wasiendelee kubaki nyuma kimaendeleo zikawafikia wanawake katika baadhi ya maeneo  hayo . Semeni ambae alijengewa uwezo akiwa kama mkulima kiongozi  TOT (Trainer of Trainers), na nafasi hiyo ikawa ngazi ya ukombozi kwake na kwa jamii yake akiwa ni miongoni mwa wanawake  4000 ,na wanufaika 16000 waliokusudiwa  kufikiwa  na mradi huo katika shehia nane Unguja na Pemba.  

Awali, Semeni anakiri kuwa haikuwa rahisi kukubali maelekezo ya kitaalamu katika shughuli zake za kilimo,wala kupanda mikoko  Lakini baada ya kupata mafunzo, aliamua kuisambaza elimu hiyo kwa wanajamii .
Haikuwa kazi rahisi kukubali mabadiliko ya mtazamo wangu mwanzoni ,nilipokuwa napatiwa mafunzo  haya ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi ,kwa haraka haraka sikuwa naona hasa ayo mabadiliko mpaka  nilipoelimishwa  nikaelewa ndipo nilipoanza kuziona zile athari zilizopo ndani ya  shehia yangu
’’Nilianza kulima kitaalamu kwa kuchanganya jamii ya miti ya mbao na matunda katika shamba moja ,huku sikubweteka  nikaanza kupambania mabadiliko ya tabia ya nchi baharini kwa kupanda mikoko na kuwashajihisha wengine  ‘’
 Ingawa tulichojifunza kupitia mradi nilitakiwa nisaidie kuisambaza elimu hiyo lakini mimi niliangalia baadae  nikisema elimu nabaki nayo siitoi jamii yangu itakuja kuwaje  nilijisambaz tangia kwa mtu mmoj mmoja  hadi sasa sikutaka nibaki nacho peke yangu, bali nimeamua kushirikisha akina mama wenzangu ili tujikomboe na umasikini kwa kupanda mikoko na kulinda mazingira yetu pamoja na kilimo mseto.
”Mafunzo haya yamezaa matunda makubwa. 
Wanawake waliopatiwa elimu sasa wamekuwa walimu wa kupanda mikoko na kuilinda, wakieneza maarifa kwa wengine ambapo kupitia mkulima kiongozi Semeni  hadi sasa jumla ya  wanawake  91  waliomuunga mkono kupanda mikoko kulinda na kusambaza elimu kwa wengine juu ya kulinda mabadiliko ya tabia ya nchiSidrat Khatib Ali, mmoja wa waliopatiwa mafunzo na Mkulima kiongozi Semeni, yeye anasema,“Urejeshaji wa mikoko umetupa matumaini mapya ya kujikomboa kiuchumi na kulinda bahari yetu yukiamini tunaanda kesho iliyobora  ya shehia yetu na vizazi vyetu. 

Tulikuwa wahanga wakubwa wa ukataji wa mikoko, lakini sasa tunaona mwanga mpya kwa vile na sisi tumekuwa mawakala wa mabadiliko hayo tunaungana kupanda mikoko na kutoa elimu ya umuhimu wa kulinda 
”Kwa upande wake, Khatib Said Khatib, mkulima mwanaume wa Mchanga Mdogo, anakiri,“Nilikuwa napanda mikoko bila utaalamu kwa muda mrefu , lakini sasa nimesimama mstari wa mbele kusaidia wanawake kila wanapokwenda kupanda mikoko,Najua baadae watanufaika wao, lakini pia kutusaidia sisi.

”Maneno haya yanaonyesha jinsi mradi ulivyobadilisha mtazamo wa jamii nzima,si wanawake pekee bali pia wanaume wameungana bega kwa bega katika kulinda mazingira ya baharini .

Mradi wa Zanz Adapt umefika katika baadhi ya  shehia ambapo kwa  upande wa Pemba ni pamoja ni shehia ya  Kambini Kichokochwe,Mjini Kiuyu ,Chwale , pamoja na Mchanga Mdogo ambazo baadhi ya sehemu ya ardhi yake imekuwa miongoni mwa maeneo yasiopungua 3000 zanzibar yalioathika kutokana na mabadiliko ya tabia ya nchi.
Katika maeneo haya, wanawake wameanza kubadilisha maisha yao kwa kupanda mikoko, kujikomboa kiuchumi, na kuwa wawakilishi wazuri wa jamii katika mapambano ya mabadiliko ya tabianchi.
Hadithi za wanawake katika baadhi ya vijiji ndani ya shehia yetu  ya mchanga mdogo , yameanza kuzaa matunda nusu na robo wanawake tumebadilika na kuimba mabadiliko ya tabia ya nchi. 
Wanawake waliopatiwa elimu sasa wanashiriki kikamilifu katika shughuli za kijamii na hata kuweza kutoa maoni yao linapotokea tatizo au wanapohitaji msaada  Wamekuwa sauti ya mabadiliko, wakihamasisha wengine kuacha ukataji wa mikoko na badala yake kushiriki katika urejeshaji wa misitu ya baharini kandaa.
CHANGAMOTO ZINAZOKABILI JITIHADA
‘’Pamoja na mafanikio haya, changamoto bado zipo,Upatikanaji wa mbegu za mikoko ni tatizo kubwa linalokwamisha kasi ya urejeshaji’’. 
‘’Aidha, uhitaji wa mafunzo ya kitaalamu zaidi ni muhimu ili kuhakikisha urejeshaji wa mikoko unakuwa wa kudumu na wa kisayansi’’,Yote hayo ni maneno ya semeni Semeni alieleza.
“Tunapanda mikoko, lakini mara nyingine tunakosa mbegu bora. Tunahitaji msaada zaidi wa kitaalamu ili juhudi zetu ziwe na matokeo ya kudumu kwa taifa la baadae.
”Changamoto hizi zinaonyesha kuwa mapambano dhidi ya mabadiliko ya tabianchi yanahitaji mshikamano wa wadau wote, serikali, mashirika ya kiraia, na jamii kwa ujumla.
Juhudi zetu zote hizi hatuoni nguvu ya serikali tunawaza mradi ukimaliza jee  nani atakuwa msaidizi wetu wa kutukomboa,na viongozi wetu hawaoni juhudi zetu wanathamini mambo mengine yasio na tija kwetu kama hawapo kabisa USHIRIKIANO NA UONGOZI WA WANAWAKE
Moja ya mafanikio makubwa ya mradi wa Zanz Adapt ni kujenga uwezo wa wanawake kushiriki uongozi Wanawake TOT wamekuwa walimu na viongozi wa jamii, wakitoa elimu kwa wenzao na kuhamasisha mshikamano wa kijamii katika kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi.
Kwa mujibu wa Jumuiya ya Uhifadhi wa Misitu Pemba (CFP), katika moja ya  maelezo yao kwa waandishi wa habari walisema kuwa  asilimia 80 ya wanawake ndio watanufaika na mradi huu  waZanz adapt huku asilima 20 ikiwa ni wanaume lengo ni kuwawezesha   wanawake kujikomboa na umasikini wa kipato kupitia kilimo mseto ,upandaji wa mikoko pamoja na usawa wa kijinisia  .
Jambo ambalo ni hatua kubwa ya katika kuimarisha nafasi ya wanawake katika mapambano ya mabadiliko ya tabianchi  hususan ni maeneo ya vijijini .
Mmoja wa viongozi wa CFP alisema Omar Tarika Msellem Akiwa katika Ukumbi wa TAMWA mwanzoni mwa ufunguzi wa mradi huu,Jitihada za Semeni na wenzake zimeleta mabadiliko makubwa ya kijamii na kiuchumi. 
Kupanda mikoko si tu kunalinda mazingira, bali pia kunatoa fursa za kiuchumi kupitia kilimo msitu, ufugaji wa samaki, na utalii wa mazingira sambamba na uanzishwji wa vikundi  ambavyo vitaunga mkono juhudi hizo.
Wanawake sasa wanajiona kama sehemu ya suluhisho, si wahanga wa matatizo. Wamepata nafasi ya kushiriki katika maamuzi ya kijamii na kisiasa, jambo ambalo awali lilikuwa changamoto kubwa kutokana na mila na desturi,ushahidi wa hilo ni kuziona sauti zao wakisemea kuhusu mabadiliko ya tabia ya nchi kupitia vyombo vya habari ,alisema Amina Ahmed Mohamed kutoka chama cha waandishi wa habari wanawake TAMWA .
Safari ya Semeni Suleiman Hamad ni ushahidi wa nguvu ya elimu na uongozi wa wanawake katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi. Kupitia juhudi zake, jamii ya Mchanga Mdogo na maeneo mengine ya Pemba sasa yana matumaini mapya ya kulinda mazingira, kujikomboa kiuchumi, na kuendeleza kizazi kinachojali uendelevu wa rasilimali za bahari na ardhi.
Semeni na wanawake wenzake wameonyesha kuwa mapambano dhidi ya mabadiliko ya tabianchi si jukumu la serikali pekee, bali ni wajibu wa kila mwanajamii. 
Kwa kupanda mikoko na kulinda kandaa, wameweka msingi wa mustakabali bora wa Pemba na Zanzibar kwa ujumla.Huku Kauli yake ya mwisho inabaki kama dira ya matumaini,“Tunapopanda mikoko, tunapanda pia matumaini ya maisha bora kwa vizazi vijavyo sisi tukishaondoka tumeyaacha mazingira ambayo yanahimili mabadiliko ya tabia ya nchi”MWISHO