Habari

Jumatatu, 9 Februari 2026

HADI KUFIKA MIAKA 62 YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR ELIMU NI HAKI SIO UPENDELEO

Na ,Amina Ahmed Moh'd
 
Kabla ya Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964, elimu ya maandalizi Unguja na Pemba haikuwa rasmi wala jumuishi. Ilitolewa kwa upendeleo wa kijamii na kikabila, na iliwafikia wachache wa tabaka la juu  maeneo ya mijini pekee.
 Watoto wa maskini, wakulima na wavuvi walikosa fursa
 Hakukuwa na skuli za serikali za maandalizi
 Vijijini, watoto walitegemea  (Madrasa)   elimu ya dini pekee
Hakukuwa na utaratibu wa lishe, walimu walikuwa wachache na wengi wageni wasio kuwa wazawa 
 Mfumo wa elimu ya maandalizi  ulikuwa wa kikoloni na kisultani, elimu ikiwa si haki ya kila ZANZIBAR 
LAKINI  BAADA YA MAPINDUZI YA 1964 – MIAKA 62 BAADAYE (2026)
Mapinduzi yameleta mageuzi makubwa katika elimu ambapo 
 Elimu ndani ya miaka 62 ya Mapinduzi  kupitia serikali ya awamu ya nane  iliyo chini ya Dk Hussein Ali Mwinyi  imekuwa ni haki ya kila mtoto bila ubaguzi wa kidini, itikadi za siasa ,uchumi ,maumbile wala hali za maisha kama ilivyokuwa kabla ya Mapinduzi  yam waka 64 .
Huku Zaidi ya skuli  262 za maandalizi Unguja na Pemba ndani  ya miaka 62 ya Mapinduzi  
 Skuli 97 zimekarabatiwa, 36 mpya zinajengwa maeneo mbali mbali .
 Walimu wapya 889 wameajiriwa ndani ya miaka 62 mwaka  (2025/26)
  Wanafunzi wapatao  105,101 (82.5%) wameandikishwa  jambo ambalo awali kabala miaka 62 ya Mapinduzi halikuwepo 
  Wanafunzi 63,099 (50%) wanapata lishe  maskulini  kupitia ruzuku maalum ya serikali  
 ZANZIBAR  YA LEO  katika elimu ina mfumo jumuishi wa elimu, miundombinu bora, walimu wenye sifa na huduma za kijamii maskulini  ,lishe  na mazingira yaliorafiki  kwa wote 
________________________________________

Miaka 62 ya Mapinduzi ya Zanzibar  kupitia serikali ya awamu ya nane inayoongozwa na Dk Hussein Ali Mwinyi ni ushahidi kuwa: Elimu si upendeleo  bali  Elimu ni haki kwa watu wa aina zote kuanzia madarasa ya awali.
Mapinduzi yameifanya haki hii kufika kwa kila mtoto wa Zanzibar popote alipo  mjini na Vijijini 


  Maono ya kiongozi bora huonekana pale elimu inapokuwa haki ya kila mmoja  huku Taifa imara hujengwa na viongozi wanaothamini elimu bila ubaguzi kwani Uongozi bora huacha alama kupitia elimu jumuishi na yenye usawa kuanzia ngazi ya awali hadi vyuo vikuu .
  


 JEE WAJUWA Kabla ya Mapinduzi (1964)
• Elimu ya maandalizi haikuwa rasmi wala jumuishi.
• Iliwafikia wachache wa tabaka la juu mijini pekee.
• Watoto wa maskini, wakulima na wavuvi walikosa fursa.
• Hakukuwa na skuli za serikali za maandalizi.
• Vijijini, watoto walipata elimu ya dini kupitia madrasa pekee.
• Walimu wachache, wengi wakiwa wageni wasio wazawa.
• Mfumo ulikuwa wa kikoloni na kisultani, elimu si haki ya kila mtoto.
Baada ya Mapinduzi (1964–2026)
• Elimu imekuwa haki ya kila mtoto bila ubaguzi wa dini, siasa, au hali ya maisha.
• Skuli za maandalizi 262 zimeanzishwa Unguja na Pemba.
• Skuli 97 zimekarabatiwa na 36 mpya zinajengwa.
• Walimu wapya 889 wameajiriwa.
• Wanafunzi 105,101 (82.5%) wameandikishwa.
• Wanafunzi 63,099 (50%) hupata lishe shuleni kupitia ruzuku ya serikali.
• Mfumo wa elimu sasa ni jumuishi, wenye miundombinu bora, walimu wenye sifa, na mazingira rafiki.
Hitimisho
Mapinduzi ya Zanzibar yamebadilisha elimu kutoka upendeleo wa kikoloni hadi haki ya kila mtoto. Leo, elimu jumuishi na yenye usawa imejengwa kuanzia madarasa ya awali hadi vyuo vikuu, ikionesha maono ya uongozi bora unaothamini elimu kwa wote.

FREELANCER  
    AMINA AHMED MOH`D – ( BIYAYA)
    0776 -859 184
    minnah1202@gmail.com

Jumapili, 8 Februari 2026

VIKOPO VYA WATU WALEMAVU WANAO OMBA BARABARANI VINADUMAZA UCHUMI WAO

 NA ASIA MWALIM

KATIKA jamii nyingi duniani, watu wenye ulemavu wamekuwa wakionekana kama kundi linalohitaji msaada wa kudumu, mtazamo huu umekuwa ukichochea dhana potofu kwamba hawawezi kujitegemea kiuchumi.
Hali hii si tofauti kwa Zanzibar, ambako baadhi ya wananchi bado wanaamini kuwa watu wenye ulemavu ni tegemezi na hawawezi kuishi bila ya vikopo vya misaada barabarani. Hata hivyo, ushahidi unaonyesha kuwa wanawake na wanaume wenye ulemavu wana uwezo mkubwa wa kujitegemea kiuchumi endapo watapatiwa mitaji, mafunzo na mazingira rafiki ya biashara.
TAKWIMU ZA WATU WENYE ULEMAVU
Viashiria ya kijamii, uchumi na mazingira vilivyojitokeza katika sensa ya watu na makaazi ya mwaka 2022, vinaonyesha kuwa Zanzibar watu wenye ulemavu kuanzia miaka 7 na kuendelea ni 114 kwa kila 1000.Ripoti inaonesha idadi ya watu wenye ulemavu imeongezeka kwa watu 39 kwa kila 1,000 kati ya sensa ya mwaka 2012 na ya 2022.
HALI YA KIUCHUMI KWA WATU WENYE ULEMAVU
Wanawake na wanaume wenye ulemavu wameanzisha biashara ndogondogo ikiwemo ufumaji wa bidhaa za mahoteli, ushonaji wa nguo na ujasiriamali. 
Hii ni ishara tosha kwamba ulemavu si kikwazo cha mafanikio ya kiuchumi.Aisha Ali Abdallah, mlemavu wa uoni ni  mjasiriamali anaetengeneza na kuuza bidhaa za vipodozi, sabuni na mafuta anajitegemea kuendesha maisha yake na mara kadhaa amekua akitoa msaada kwa wazazi wake.anasema ni vyema kuwekwa mazingira rafiki ya biashara hasa kupatiwa mitaji na masoko ili kukuza uchumi wao bila kutegemea misaada.“Changamoto kubwa inayotukabili watu wenye ulemavu ni ukosefu wa mitaji, bila ya mitaji, hata wazo bora la biashara haliwezi kutekelezwa” anasema.
Ili kupiga hatua za kimaendeleo anasema ni vyema kuhamasisha jamii kupitia vyombo vya habari kuhusu uwezo wa watu wenye ulemavu, anashauri serikali Kushirikisha jumuiya za watu wenye ulemavu katika kutunga sera na mipango ya maendeleo.Fatma Ali, Mjasiriamali Mlemavu wa Miguu ameanzisha biashara ya ushonaji nguo katika eneo la Mwera, Unguja. Biashara yake imekua na sasa anatoa ajira kwa wanawake wengine, wakiwemo wenye ulemavu.Anasema anafanya kazi kwa kutumia mashine za kushona na hujipatia kipato cha kutosha kuendesha maisha bila kutegemea misaada.
MITAZAMO YA JAMII
Hanifa Mohammed Said anasema, umefika  wakati jamii kuachana na dhana walioijenga muda mrefu kuwa watu wenye ulemavu ni kundi linalohitaji msaada wa kudumu.Anashauri seriakali kuandaa mikakati ya kuona wadau na wahisani wenye uwezo kuwapa mitaji ya kuwawezesha ili kufanya biashara na shughuli za kuwaingizia kipato ili kukidhi mahitaji yao ya kila siku na sio kuwapa chakula cha siku chache kisha kukosa shughuli za kufanya.“Wanahitaji kupatiwa mitaji ya kufanya kazi zenye muendelezo wa kukuza uchumi wao ili kuondokana na kadhia ya kila siku kupokea msaada mdogo ambao hauwezi kukidhi mahitaji zaidi ya siku tatu kwenye familia zao” anasema.Khamis Saleh Khamis anaeleza kuwa hali ya sasa imesababisha baadhi ya wananchi kuamini watu wenye ulemavu hawawezi kujitegemea kiuchumii, jambo ambalo si tu linawadhalilisha bali pia linazuia fursa za maendeleo kwa watu hao.“Mitazamo ya jamii kwamba watu wenye ulemavu ni tegemezi imejengwa kwa miaka mingi kutokana na ukosefu wa elimu na uelewa” anasema. Mwanakheri Rajab Hilali anasema iIli kubadilisha mitazamo mibaya kwa jamii elimu inahitajika kubainisha uwezo wa watu wenye ulemavu na kuimarishwa kupitia vyombo vya habari, mashule, na taasisi za dini.Anasema ushirikishwaji wa watu wenye ulemavu katika shughuli za kijamii na kiuchumi unapaswa kupewa kipaumbele, pamoja na kuonesha mafanikio ya wafanyabiashara wenye ulemavu kama mfano wa kuigwa.
JUMUIYA YA WANAWAKE WENYE ULEMAVUMwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake wenye Ulemavu Zanzibar Salma Haji Saadat, anasisitiza jamii kuwatizama watu hao katika mtizamo chanya kuona kwamba wanaweza kuleta mabadiliko katika kuchangia mapato ya nchi na kukuza uchumi wao.“Tunashuhudia watu wenye ulemavu wakiwa na vikopo vyenye rangi moja wakiomba pesa katika maeneo mbali mbali ya zanzibar hili sio jambo jema na linasikitisha hasa kutokana na mila na desturi za Kizanzibari” anasema.Anasema watu wenye ulemavu wana uwezo wa kufanya kazi kama ilivyo watu wengine au zaidi ya watu wa kawaida kutokana na uwezo waliobarikiwa.“utawakuta Watu wenye ulemavu wametapakaa kila kona hasa maeneo ya mjini wakioneka kazi yao ni kuomba tu ili kupata kipato chao bila ya kuangalia uwezo wao wa kazi” anasemaAnasema miongoni mwa changamoto zinazowakabili watu wenye ulemavu ni kukosa masoko, mikopo ya 4.4.2 ili kujiendeleza kuichumi.Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania-Zanzibar (TAMWA)Afisa Programu na Mawasiliano Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania-Zanzibar (TAMWA) Khairat Haji anasema TAMWA kwa kushirikiana na taasisi mbali mbali imewezesha watu wenye ulemavu kuanzisha miradi ya sabuni za maji, vipodozi, ushonaji wa mikoba na nguo, na kilimo cha mboga za majani ili kunyanyua uchumi wao.Anatolea mfano mradi wa Kijaluba Isave, ulioendeshwa na TAMWA Zanzibar kwa kushirikiana na SHIJUWAZA, ambao watu wenye ulemavu wamewezeshwa kuunda vikundi vya kuweka na kukopa ili kukuza uchumi wao na kuacha kuwa tegemezi.(WAKALA WA UWEZESHAJI WANANCHI KIUCHUMI ZANZIBAR (ZEEA) inasema imechukua hatua za kuwawezesha watu wenye ulemavu kwa kutoa mikopo kwa masharti nafuu, kutoa mafunzo ya ujasiriamali na usimamizi wa fedha.Kwa mujibu wa taarifa za ZEEA, takriban watu wenye ulemavu 170 wamepatiwa mikopo ya 4.4.2  kuanzia mwaka 2024 hadi sasa.Kati yao wanawake 93 na wanaume 79 hatua inayolenga kuondoa utegemezi wa misaada ya huruma na kuwezeshwa kiuchumi.SHERIA,MIKATABAKuhusu uwezeshaji wa kiuchumi kwa watu wenye ulemavu, Tanzania ina mwongozo kupitia Sheria ya Watu Wenye Ulemavu ya mwaka 2010 (Persons with Disabilities Act, 2010).sheria hiyo inaeleza kuwa kila mtu mwenye ulemavu ana haki ya kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi,kijamii na kisiasa.serikali na mamlaka husika zitahakikisha kuwepo kwa sera, programu na mikakati ya kuwawezesha watu wenye ulemavu kupata ajira, mikopo,mafunzo ya ujuzi, na fursa nyengine za kujipatia kipato, bila ubaguzi wowote kutokana na hali ya ulemavu.Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Watu Wenye Ulemavu (CRPD, 2006)Kifungu cha 27: Kinahusu Haki ya Kazi na Ajira. Kinaeleza kuwa watu wenye ulemavu wana haki ya kufanya kazi kwa uhuru, kuchagua ajira wanayoipenda, na kufanyiwa mazingira rafiki bila ubaguzi.Kifungu cha 28: Kinahusu Haki ya Kiwango Bora cha Maisha na Ustawi wa Kijamii, ikiwemo upatikanaji wa huduma, mikopo, na fursa za kiuchumi.Nchi wanachama (ikiwemo Tanzania) zinapaswa kuweka sera na programu za kuwawezesha kiuchumi, ikiwemo mafunzo ya ufundi, mikopo midogo, na ajira zenye staha.

ATHARI ZA KUTOWASHIRIKISHA WATU WENYE ULEMAVU KWENYE NGAZI ZA MAAMUZI

.NA, ASIA MWALIM NCHI nyingi hupanga mipango yake ya Kimaendeleo na kiuchumi kwa kuzingatia mambo mengi.Hii ni pamja na idadi ya watu wake na zaidi mahitaji yao, ikiwa pamoja na kuzingatia maumbile.
Katika hayo mazingatio limo kundi la watu wenye mahitaji maalum katika maisha yao ya kila siku na miongoni mwao ni wale wenye ulemavu. 
Takwimu za Umoja wa Mataifa zinaonesha takriban asilimia 15 ya watu duniani ambao ni zaidi ya bilioni moja ni wenye ulemavu, wengi wakiwa wanawake. Hata hivyo, kundi hili bado halijapewa umuhimu unaostahiki katika baadhi ya maeneo, hali inayowanyima haki zao za kikatiba na kidemokrasia.
 Miongoni mwa malalamiko yanayosikika hapa kwetu ni ya vyama vya siasa kushindwa kuwasimamisha watu wenye ulemavu majimboni na badala yake kutegemea nafasi za viti maalumu pekee. Wapo wanaouliza kama Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama.Samia Suluhu Hassan na Rais wa Zanzibar,Dk.Hussein Ali Mwinyi, wanawaingiza wanawake wenye ulemavu katika uteuzi wao kipi kinachofanya hali kama hiii kushindikana katika vyama vya siasa kuwaweka  kuwa wagombea katika uchaguzi? Matokeo ya sensa yanaonesha kiwango cha watu wenye ulemavu Tanzania kimeongezeka kutoka watu 93 katika mwaka 2012 hadi 112 mwaka 2022 kwa kila watu 1,000. 
Katika miaka ya karibuni Zanzibar imeshuhudia serikali ikiteua wanawake zaidi, wakiwemo wenye ulemavu katika nafasi za juu za uongozi. Katika mahojiano maalum wanawake wenye ulemavu walielezea wanavyotamani kuipata haki ya kuchaguliwa kwenye majimbo kwa njia nyepesi, kama ilivyo kwa watu wengine. Vyama vya siasa havijatoa umuhimu wa kusimaisha watu wenye ulemavu majimboni na hili limelezewa na wanwake wenye ulemavu kama ni ubaguzi.
 Jamila Borafya wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) alisema kundi hilo lina uwezo wa kuongoza nafasi za uwakilishi au ubunge majimboni na sio tu kupitia nafasi za viti maalumu. "Tunataka nafasi za majimboni na sio za viti maalumu pekee kwani tunao uwezo na uzoefu wa kutosha" alisema. Alisema ni vizuri wanawake wenye ulemavu wanapojitokeza kugombea wakapewa nafasi sawa na wagombea wengine na hata kuwapa kupaumbele.

Alisema mtindo wa sasa wa kutoa zaidi nafasi kwa wanaume sio sahihi na unahitaji marekebisho. 
Adil Mohammed Ally, Mratibu Jumuiya ya Wasioona Zanzibar (ZANAB), alisema watu wenye ulemavu wana himili kuongoza nafasi za majimbo, lakini ipo haja kwa vyama vya siasa kuzingatia hilo ile watu hao wapate haki yao ya kikatiba. Alishauri Tume ya uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) kuweka sheria madhubuti na msisitizo kwa vyama vya siasa kutoa kipaumbele kwa watu wa kundi hili watapotaka kugombea majimboni. Hata hivyo, aliwataka watu wenye ulemavu kujitokeza kwa wingi majimboni mwaka 2025 kwani jamii imebadilika na yamefanyika marekebisho ya mifumo ya kupiga kura kwa watu wenye ulemavu. Alitoa mfano wa katiba ya Zanzibar ya 1984, ambayo inaeleza katika kifungu 21(2) kila Mzanzibari anayo haki na uhuru wa kushiriki ukamilifu katika kufikia uamuzi wa mambo yanayomuhusu yeye na taifa. Vile vile katika marekebisho ya 2010 katiba imeeleza katika kifungu nambari 67 (1) kuwa kutakuwa na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wanawake kwa asilimia 40 ya wajumbe wakuchaguliwa katika majimbo. Aisha Ali Abdallah, kutoka ZANAB aliyeshiriki kugombea nafasi ya uongozi wilaya ya Chake chake, Pemba, alisema ushiriki wao katika kugombea nafasi za uongozi ni mzuri,lakini vyama vya siasa haviwapi nafasi. 
"Nilishiriki kugombea uwakilishi katika uchaguzi wa mwaka 2020, lakini sikuipata hiyo nafasi" alisema. Alisema hadi sasa Pemba hakuna kiongozi mwenye ulemavu ambaye wanaweza kumpa changamoto za kutatua matatizo yao kwa wakati. VIONGOZI WENYE ULEMAVU Mwantatu Mbarouk Khamis, Mwakilishi wa viti maalum kupitia Chama Cha Mapinduzi, (CCM) alisistiza haja ya wana siasa kuwaunga mkono watu wenye ulemavu kwa kuwapa nafasi majimboni ili waweze kushiriki katika vyombo vya maamuzi. Hadi kukamilika uchaguzi 2020, Katika Baraza la Wawakilishi kuna viongozi watatu tu waliopata nafasi hizo kupitia viti maalumu kwa tiketi za CCM. "Mwanamke mwenyewe ulemavu anao uchungu wa kusaidia jamii yake kupata maendeleo na hakuna sababu ya kuweka matabaka, Sote ni viumbe hatujakamilika, kila mtu ni mlemevu mtarajiwa" , aliongeza. VIONGOZI WA MAJIMBONI Mbunge wa Kiembesamaki, Mohammed Maulid, alisema jamii inapaswa kuwapa nafasi wanawake na watu wenye ulemavu kwani ni baraka na kuwakwamisha ni kutowatendea haki.Diwani wa Fukuchani, Fatma Ngwali Khamis, alisema licha ya hali yake na kukumbana na changamoto alishinda kupitia kura za wananchi kutokana na uwezo wake wa kuongoza na kuwataka watu wenye ulemavu kujitokeza zaidi majimboni licha ya magumu wanayopitia. Alisema wapo wanaodhani ukimuweka mtu mwenye ulemavu jimboni ni kama kupoteza nafasi, dhana iliyobebwa na jamii kubwa hasa wanasiasa. 
WANAHARAKATI 
Aliekua Mkurugenzi wa Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania TAMWA-ZNZ, Dk.Mzuri Issa, alisema licha ya jitihada zinazofanyika zipo changamoto wanazopata wanawake na watu wenye ulemavu kufikia malengo yao. Miongoni mwa changamoto ni baadhi ya viongozi wa dini, jamii na vyama vya siasa hawajaweka umuhimu kwa wanawake na watu wenye ulemavu kupewa nafasi za uongozi. Alisema wakati mwengine watu wenye ulemavu wanabezwa na kufanyiwa dhihaki kwa kuangaliwa hali zao na kipato chao na kuitaka jamii kubadilika. Alishauri sera na sheria za vyama vya siasa kusisitiza usawa kwenye nafasi za uongozi na maamuzi na kuvitaka vyombo vinavyohusika kusimamia haki. Vyombo hivi nipamoja na Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar (ZAECA) kuweka mustakabali mzuri kwa makundi yote.Ukhty Amina Salum, alisema sio sahihi kutumia dini kama kigezo cha kumzuia mwanamke kuongoza, kwani dini inatambua uwezo wa mwanamke kuongoza. Bi Asha Abdi, Mwenyekiti wa Mtandao wa Jinsia Zanzibar, alisema kuna umuhimu wadau na wanaharakati kulifanyia kazi sula la watu wenye ulemavu, hasa wanaogombea uongozi. TUME YA UCHAGUZI YA ZANZIBAR (ZEC) Mkurugenzi wa Uchaguzi Zanzibar, (ZEC)Thabit Idarous Faina, alisema kazi ya tume ni kupokea maombi ya wagombea waliopitia mchakato katika vyama vyao. Lakini ili kuondosha upendeleo usio wa lazima ni vizuri kwa vyama vya siasa kuliangalia hili kjwa undani ili kuondoa tataizo liliojitokeza.
 Alisema tatizo la usimamizi wa wagombea ni kwa vyama kutowasilisha majina ya agombea mapema ili kuhakikisha asilimia 40 ya wanawake wagombea inafikiwa. Alisema katika kueleka uchagyzi wa 2025, ZEC itaendelea kushirkiana na vyama vya siasa ili kupambana na rushwa na kuhakikisha wanawake wanapewa kipaumbele ili waweze kushiriki kwa asilimia kubwa zaidi. Kwa hali ilivuo sasa suala la vikwazo ambavyo wanawake na watu wenye ulemavu wanapambana navyo wanapoamua kugombea nafasi za uongozi ni tatizo inalohitaji kufanyiwa kazi ya ziada.
 IDARA YA WATU WENYE ULEMAVUKatibu Mtendaji wa Baraza La Taifa la Watu wenye ulemavu Zanzibar, Ussy Khamis Debe, alisema ni vyema Tume ya uchaguzi na mabaraza ya vyama vya siasa kuweka mazingira rafiki ya watu hao kupata nafasi hizo.Aliitaka jamii na vyama vya siasa kuacha kuwatenga na kutokana na dhana potofu zinazotumika kuwazuwia wanawake na watu wenye ulemavu wasigombee uongozi. 
JUMUIYA YA WANAWAKE WENYE ULEMAVU ZANZIBAR (JUWAUZA) Mkurugenzi Mtendaji Jumuiya ya Wanawake Wenye Ulemavu Zanzibar, Bakar Omar Hamad, alieleza kuwa watu wenye ulemavu na hasa wanawake wanapitia wakati mgumu wanapotamani kuwa viongozi. Katika mwaka 2020 kupitia vyama vya siasa takriban watu wenye ulemavu 30 walijitokeza kugombea nafasi tofauti majimboni na mwanamke mmoja mwenye ulemavu alishinda nafasi ya udiwani kati ya majimbo yote 50 ya Unguja na Pemba. Mwenyekiti wa Baraza la Watu Wenye Ulemavu, Salma Haji Saadat, alisema vyama vya siasa vinao wajibu wa kuhakikisha watu wenye ulemavu wanapewa kipaumbele katika nafasi za uongozi.
 Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Zanzibar, Abeda Rashid alisema licha ya changamoto zinazowagusa wanawake, lakini wamenufaika na fursa fursa hizo katika miaka ya karibuni.Abeda alisema kuna nafasi muhimu katika taasisi za serikali zinazoshikiliwa na wanawake. Miongoni mwao ni ya yeye amabye ni mwenye ulemavu kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii. Aliwapongeza wadau maendeleo na taasisi mbali mbali ikiwemo WILDAF, TAMWA, JUWAUZA, kwa kuwa mstari wa mbele kuwashirikisha wanawake kwenye mafunzo ya kuwezesha kushika nafasi za uongozi.
 MATAMKO MBALIMBALI YALIOLENGA USAWA Dira ya maendeleo ya Zanzibar ya mwaka 2050 imekusudia kuongezeka kwa fursa kwa makundi ya watu wasiojiweza wakiwemo watu wenye ulemavu, wanawake watoto na wazee. Itifaki ya Jumuiya ya Maendeleo ya nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) mkataba wake wa kikanda uliotiwa saini mwaka 2008 na nchi wanachama wake ikiwemo Tanzania, wenye vifungu 43 unaelekeza nchi hizo kuzingatia suala la haki na usawa kati ya wanaume na wanawake katika suala la uongozi. Kwa muhtasari ipo haja ya kulifanyia tathmini suala hili ili kuhakikisha watu wenye ulemavu na hasa akina mama wanatendewa haki na jamii yetu. Kwa muda mrefu na hadi sasa umepatikana uthibitisho wa kutosa wa kuonyesha uwezo wa watu wneye ulemavu, wanaume na wanawake, kushika hatamu na kuwa viongozi wa kupigiwa mfano.Moja ya njia ya kuliondoa tatizo hili ni kuongeza idadi yao kupitiamajimbo kwani hii itasaidia kupaza sauti zao kwenye vyombo vya maamuzi, hasa wakati wa kutungwa sera mbali mbali. 
Mwisho

Jumanne, 3 Februari 2026

MAENDELEO YA YA ELIMU YA MAANDALIZI NDANI YA MIAKA 62 YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR YAKUPIGIWA MFANO,,NEEMA KWA WOTE BILA UBAGUZI

 AMINA AHMED  MOHD

  JEE !  WAJUWA KABLA      Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964, elimu ya maandalizi  ndani ya visiwa vya unguja na Pemba  haikuwa rasmi, na nathubutu kusema haikuwepo kabisa ! hukukatika maeneo iliyokuwepo  ilitolewa kwa upendeleo wa kijamii na kikabila, na watoto wengi wa tabaka la chini watoto wa mskini, wakwezi na wakulima  hawakupata nafasi ya kujiunga na skuli za maandalizi ,huku Elimu ikibaki kuwa ya kikundi kidogo cha watotokutoka familia za wenye uwezo  na si haki ya kila mtoto.Yote hayo sababu kubwa ilikuwa Mfumo wa elimu ulikuwa ni wa kikoloni na wakisultani, ukilenga zaidi watoto wa tabaka la juu mijini, huku vijijini kukikosekana kabisa huduma za elimu ya awali ambayo kwa sasa inatambulika kama elimu ya maandalizi .HISTORIA YA ELIMU YA MAANDALIZI ZANZIBAR KABLA YA MAPINDUZI  YA ZANZIBAR YA MWAKA 64  UPATIKANAJI WA ELIMUElimu ya maandalizi haikuwa sehemu ya sera ya serikali ya kisultani. Hakukuwa na mtandao wa  skuli  za serikali kwa watoto wote; badala yake  skuli nyingi zilikuwa za binafsi na nyentine zikiwa  kidini.Elimu ya awali haikujulikana kwa kiwango cha kitaifa, bali ilikuwa ni ya kikundi kidogo cha watu wenye uwezo na maeneo yaliyokuwa rafiki kufikika maeneo ya unguja mjiniWatoto wachache wa tabaka la juu, hasa wa asili ya Kiarabu na kiswahili wa mjini, ndio waliopata nafasi ya kujiunga na skuli za awali,huku Vijijini, watoto walitegemea madrasa na elimu ya dini kama njia pekee ya skuli za maandaliz katika kujifunza .Mfumo wa elimu ulikuwa wa kikoloni na kisultani, ukilenga zaidi watoto wa tabaka la juu.Skuli  chache zilikuwepo, nyingi zikiwa mijini na hazikuwafikia watoto wa vijijini.Elimu ya maandalizi haikuwa rasmi, watoto wengi walijifunza kupitia madrasa au elimu ya jadi.Uwiano wa walimu kwa wanafunzi ulikuwa duni, walimu wachache na wengi wakiwa wageni.Huduma za kijamii skulini  hazikuwepo, hakuna lishe shuleni wala ruzuku kwa wanafunzi.Uandikishaji ulikuwa mdogo sana, idadi kubwa ya watoto wa Zanzibar hawakupata nafasi ya kusoma elimu ya maandalizi . Walimu wachache walikuwepo, wengi wakiwa wageni au wa tabaka la juu.Idadi ya watoto waliopata elimu ya maandalizi ilikuwa ndogo sana, ikilinganishwa na idadi ya watoto wa Zanzibar.Hakukuwa na mafunzo maalum ya ualimu wa maandalizi; walimu walitegemea uzoefu wa madrasa au elimu ya msingi ya kikoloniELIMU BAADA YA MAPINDUZI  1964–  ILIPOFIKIA MIAKA 62   MWAKA HUU 2026)Kuna mageuzi makubwa  mabadiliko na maendeleo ya elimu  yamefikiwa  miongoni mwa hayo ni pamoja na Elimu sasakuwa  haki ya kila mtoto,kwa lazima  bila ubaguzi wa kijamii,dini siasa wala  uchumi . Kabla ya Mapinduzi ya mwaka 1964, elimu ya maandalizi Zanzibar haikuwa rasmi, haikuwa jumuishi, na iliwafikia wachache tu wa tabaka la juu mijini. Mapinduzi ya Zanzibar yalibadilisha hali hii kwa kuifanya elimu kuwa haki ya kila mtoto bila ubaguzi, na kuanzisha mtandao wa shule za maandalizi na msingi unaofadhiliwa na serikali. Skuli zimeongezeka kwa kasi ndani ya miaka 62 ya Mapinduzi  ya mwaka 1964  Kwa sasa kuna zaidi ya 262 za maandalizi  zinazopata ruzuku ya Serikalikatka kutoa huduma bora kwa wananchi za serikali na binafsi ..Ndani ya miaka 62 ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar kuna Ukarabati na ujenzi mpya: Skuli 97 za maandalizi zinazojumuisha na a msingi zinaendelea kukarabatiwa, na ujenzi wa shule mpya 36 (21 za maandalizi, 15 za msingi)ukiendelea katika maeneo mbali mbali Unguja na Pemba.Ongezeko la Walimu wapya,889 wamepangiwa kazi  mwaka 2025/26  pekee, wakisaidia kupunguza uwiano wa walimu kwa wanafunzi jambo ambalo kabla ya miaka 62 ya mapinduzi ya  ya 1964 hayakuwepo .Kuna ongezeko la Uandikishaji wa Wanafunzi , Wanafunzi 105,101 sawa na asilimia  (82.5%) wameandikishwa katika skuli  maandalizi maeneo yote  Unguja na Pemba hadi kufikia miaka 62 ya mapinduzi matukufu ya Zanzibar yalioasisiwa na  Hayat mzee Abeid Aman Karume .Ambapo huduma  za lishe Maskulini kabla ya miaka  ya Miaka 62 ya Mapinduzi ya Mwaka 1964 hazikuwepo kabisa lakini kwa  ndani ya miaka 62 ya Mapinduzi hayo Matukufu   huduma za lishe zimeongezeka na kufikia asilimia  50  na wanafunzi    wapatao 63,099 .hupata lishe bora kupitia ruzuku ya serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.  Sekta ya elimu ya maandalizi na msingi Zanzibar imepiga hatua kubwa baada ya Mapinduzi ya mwaka 1964, ikilinganishwa na hali ya elimu kabla ya Mapinduzi. Leo, miaka 62 ya Mapinduzi hayo  hku idadi ya mageuzi na mabadiliko katika upatikanaji wa Haki hiyo  zikionesha  kuongezeka kupatikana huduma  bora za elimu ya maandalizi  kwa uandikashaji wa wanafunzi bila ubaguzi wa aina yeyote, Lishe, elimu bora, waalimu , majengo  bora ya kupata elimu Mapinduzi yam waka 1964 hadi kufika kilele cha miaka 62 mwaka huu 2026 january 12  kumekuwa na mageuzi makubwa katika elimu ya maandalizi na msingi kutoka mfumo wa kikiloni uliokuwa wa kibaguzi na wenye  upatikanaji mdogo wa utoaji elimu  ufinyu wa maeneo ,lishe ,uwandikishaji duni na matabaka wa waalimu wachache mitaala isyorasmi hadi sasa  kuwa kasi ya mageuzi  kutoka kadhia hizo na kuwa  Zanzibar ya miaka 62 ya mapinduzi yenye  mfumo mjumuishi wa elimu ,takwimu thabiti za uandikishaji zenye kuangalia hali za wananchi,waalimu  bora, miundombinu bora  huduma za kijamii  skulini   yote hayo ni mafanikio  ya miaka 62 y MapinduizI ya Zanzibar   katika kuinua maisha ya wananchi kupitia elimu bora ambayo ndio ufunguo wa mafanikio ya taifa na mtu mmoja mmoja baadae

Jumamosi, 31 Januari 2026

BINAADAMU NA MCHANGO WA MABADILIKO YA TABIANCHI.


Na,TIME KHAMIS PEMBA.
  Binaadamu wana mchango mkubwa katika mabadiliko ya tabianchi, hasa kupitia shughuli zao za kila siku. Mabadiliko ya tabianchi yanamaanisha mabadiliko ya muda mrefu katika hali ya hewa kama ongezeko la joto duniani, mabadiliko ya mvua, na matukio ya hali ya hewa ikiwemo jua kali. 
Jinsi binaadamu wanavyochangia Matumizi ya nishati ya mafutakuchoma makaa ya mawe, mafuta ya petroli na gesi asilia (kwa usafiri, viwanda, na umeme) hutoa gesi chafuzi kama  kobondiaxyde  (CO₂) ambazo zinaongeza joto duniani. 
Ukataji wa misitu unofanywa na Binaadamu huchangia kwa kiasi kikubwa mabadiliko hayo kwani kuwepo kwa misitu husaidia kunyonya CO₂, na  inapokatwa, uwezo huo hupungua na gesi chafu  huongezeka. Kwenye shughuli za Kilimo na ufugaji baadhi ya mbinu za kilimo na ufugaji hutoa gesi kama methani (CH₄), hasa kutoka kwa mifugo ambayo nayo huchangia kupatikana na mabadiliko tabia nchi kama gesi hiyo haikuwa na udhibiti. Aidha Uzalishaji wa taka taka  ovyo zikioza bila kudhibitiwa hutoa gesi chafuzi na Athari za mabadiliko ya tabianchi huongezeka kwa joto na ukame ,mafuriko na mvua zisizotabirika,kupungua kwa uzalishaji wa chakula,Athari kwa afya ya binadamu na viumbe hai               SULUHISHO NA HATUA ZA KUCHUKUA Kutumia nishati mbadala (jua, upepo, maji),kupanda miti na kulinda misitu, kuboresha mbinu za kilimo endelevu,kupunguza taka na kusindika upya (recycling),kuelimisha jamii na kuhimiza sera rafiki kwa mazingira kwa kifupi, binaadamu ni sehemu ya tatizo lakini pia wanaweza kuwa sehemu ya suluhisho kwa kuchukua hatua zinazolinda mazingira.       
   MOJA YA MBINU ZA KUZUWIA ATHARI HIYO Mradi ZanADAPT
 ni mpango wa utekelezaji unaolenga kusaidia jamii za Zanzibar kupambana na athari za mabadiliko ya tabia nchi kwa njia ya kujenga ustahimilivu wa mazingira, kijamii na kiuchumi, hasa kwa wanawake na familia zao.                
       MRADI  HUO  UNAVYOSAIDIA: 
 Kujenga ustahimilivu wa mazingira kupitia njia za asili na za mitaaMradi unatumia mbinu za nature-based adaptation (urejesho wa mazingira), kama vile: Kulinda na kurejesha misitu ya mikoko, ambayo husaidia kupunguza athari za hali ya hewa kama mafuriko, kuzuia ukame, na kuhifadhi vyanzo vya uhai pwani.  
Misitu ya mikoko pia huingiza gesi chafu kama dioksidi ya kaboni, hivyo kuchangia kupunguza mabadiliko ya tabia nchi.  Kilimo mseto na kilimo chenye ustahimilivu wa hali ya hewa, ambacho hutoa chakula na kipato kwa wakazi huku kinapambana na athari za mabadiliko ya tabia nchi. 
 Kuendeleza mazao na mbinu za kilimo rafiki kwa mazingira ili kuimarisha ardhi na kuongeza ustawi wa ardhi kwa wakati wa mvua nyingi au ukame.        
  MBINU NYENGINE ZINAZOTUMIWA NA MRADI.  
  Uwezeshaji wa wanawake na utekelezaji wa kijamii ,moja ya malengo makuu ya mradi ni kuongeza ushiriki na uongozi wanawake katika shughuli za kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi, Kuwawezesha wanawake kupata ujuzi na nafasi za uongozi kwenye juhudi za kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na usimamizi wa rasilimali. 
 Kuunda vikundi vya wanawake wanaojifunza na kushirikiana kuhusu mbinu za kilimo, uhifadhi wa misitu, na maamuzi ya utunzaji wa ardhi.  
Kupitia mradi, wanawake wengi wameweza kushika nafasi za uongozi ndani ya vikundi vya wakulima na utekelezaji wa shughuli za mazingira.   Kujenga uwezo na elimu kuhusu mabadiliko ya tabia nchiZanADAPT inajenga uwezo kwa kutowa mafunzo kwa wadau. Mafunzo na uhamasishaji wa wakazi kuhusu mabadiliko ya tabia nchi, jinsi ya kuyakabili, na umuhimu wa kutunza mazingira kwa ustawi wa maisha yao.  Kupitia vikundi vya wakulima, wadau hupata ujuzi wa mbinu rafiki za kilimo na usimamizi wa maliasili.  
Mradi pia unalenga kuboresha ufahamu wa kijamii juu ya usawa wa kijinsia na nafasi za wanawake katika juhudi za kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.            USHAHIDI WA HILO  MRADI 
wa usawa wa kijinsia, utunzaji wa mazingira na ustawi wa kijamii na kiuchumi ‘Zanz Adapt’ umewapa mafunzo ya ujasiriamali wa kusarifu bidhaa mashambani wanawake wa shehia zilizofikiwa na mradi huo. Shehia hizo ni  Chwale, Kiuyu, Mchangamdogo na Kambini Wilaya ya Wete ambapo mafunzo yaliyotolewa ni pamoja na upikaji wa sambaro la embe, chai masala, utengenezaji wa makwaru ya ndizi na pilau masala ambazo zinatokana na mazao yanayolimwa kupitia kilimo msitu. 
Anazungumza na Mwandishi wa Makala hii Afisa kilimo msitu  na usawa wa kijinsia  kutoka taasisi ya CFP Sada Juma Segeja amesema hatua hiyo ni miongoni mwa kuwawezesha wanawake wa vijijini  kufikia fursa mbalimbali za kiuchumi na kujipatia kipato. Analifahamisha lengo la kufanya mafunzo hayo  ni kuongeza thamani  ya zao la ndizi, maembe kwa kufanya achari, viungo (spices) ambayo ni katika mazao yanayolimwa katika kilimo msitu  na kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.“Katika kufanya harakati hizi za ujasiriamali zitasaidia kukata miti ya mikandaa kwa shughuli za kujipatia kipato, yanayochangia maji kupanda juu , kuuwa mazalio ya samaki na kukosekana kwa mvua na kusababisha mabadiliko ya tabia nchi”alisema.
JEE NAO WASHIRIKI WA MAFUNZO WANASEMAJE
Washiriki wa mafunzo hayo Maryam Mbarouk  Khamis na Subeha  Suleiman Sultan walisema mafunzo hayo yatawakomboa  kiuchumi na kimaisha huk  wakivitaka vyombo vya habari kuhakikisha wanazisemea changamoto zao zinazorejesha nyuma maendeleo ya maisha yao. Mafunzo hayo ya usarifu wa mazao ni miongoni mwa utekelezaji wa mradi wa usawa wa kijinsia, utunzaji wa mazingira na ustawi wa kijamii na kiuchumi Zanz Adapt unaotekelezwa Chama cha waandishi wa habari TAMWA, wanawake Zanzibar CFI na jumuiya ya misitu  ya jamii Pemba CFP kwa ufadhili wa serikali ya Canada.     
MATOKEO YA MRADI HADI SASA 
Kwa mfano, matokeo yaliyorekodiwa (kabla ya 2025) ni pamoja na Kuunga mkono wanawake wasiopunguwa  14000  (hasa wanawake) katika kufanya kazi za kulinda mikoko, kuanzisha kilimo cha mseto, na usimamizi endelevu wa ardhi.  Kuunda vikwazo vya mafunzo vya wakulima kwa mazoea ya hali ya hewa,kushiriki wanawake zaidi katika maamuzi ya kijamii na mazingira ndani ya jamii .
Mradi ZanADAPT unasaidia kupambana na mabadiliko ya tabia nchi kwa kuhifadhi na kurejesha misitu ya mikoko kwa ustawi wa mazingira, kuendeleza kilimo chenye ustahimilivu wa hali ya hewa.    Kukuza ujuzi na uwezo wa jamii kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi, kuinua wanawake kiuchumi na kijamii katika juhudi za kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa.             
         MKUFUNZI KUTOKA MRADI WA ZAN ADAPT .
 Ofisa kutoka mradi wa ZanAdapt Meiya  Mbarouk Mussa alisema endapo wanawake   watajishughulisha na ujasiriamali wataweza kujikomboa katika hali duni na kuweza kuongeza kipato kitakachowakimu katika maisha yao.“Niwaombe munapotayarisha bidhaa zenu kufuata sheria ikiwemo ya usafi binafsi na eneo husika, usalama na uhakika wa munachokizalisha kufanya hivyo mutapata mafanikio na mutajiwezesha zaidi”, alisema.Aidha kwa vile Binaadamu mwenyewe ameshafahamu juu ya uharibifu anaofanya unavyomuathiri kimazingira wameanza kuchukuwa juhudi ya kuhifadhi mazingira kwa kukabiliana na tabia nchi .Kikundi cha Uhifadhi wa Mazingira katika kiji cha Shengejuu mkoa wa Kaskazini Pemba kimeamuwa kupanda miti ya mikoko ipatayo elfu kumi kwa ajili ya kukabiliana na mabadiliko tabia nchi.             
    JAMII NA TAASISI ZA KIMAZINGIRA.
Katibu wa kikundi hicho Hamad Omar Salim akizungumza na Makala hii anasema wameamuwa kufanya hivyo baada ya kuona mashamba ambayo walikuwa wanayatumia kwa kilimo cha Mpunga huko katika eneo la Ambasha Shengejuu kuvamiwa na maji ya Chumvi na hivyo kuwakosesha wananchi kupata eneo la Kilimo.‘’ Mwanzo eneo hili wazazi wetu walilitumia kwa kilimo lakini baada ya wanaadamu wenyewe kuliathiri kwa kukata miti , ya mikoko na majani mengine makubwa yaliokuwa yanahifadhi maji yasipande juu tumekuwa na athari kubwa sana’’, anasema.Katibu wa jumuiya ya uhifadhi wa mazingira ( JIKEUMA) Kisiwa panza wilaya ya Mkoani Pemba Juma Ali Mati wakati anazungumza na mwandishi wa Makala hii anasema ene la Kisiwa panza limeathirika sana na mabadiliko tabia nchi kutokana na matumizi mabaya yanayofanywa na binaadamu mwenyewe ikiwemo kukata mikoko na kuchukuwa mchanga sambamba na Sunami iliathiri maeneo mengi ya Kisiwa cha Pemba. Anaeleza kuwa kutokana na athari hizo za mabadiliko tabia nchi jumla ya familia 100 zimekosa sehemu za kilimo na hivyo walitumia shilingi milion 500 ambazo walipatiwa kupitia mfuko wa kusaidia nchi maskini.Hata hivyo anasema fedha hizo zilitumika kwa kupunguza uharibifu wa maeneo yalioathiriwa na mabadiliko tabia nchi lakini sio kuondosha tatizo hilo , hivyo Binaadamu anawajibu wa kuhakikisha anapambana kwa kila hali ili kudhibiti mabadiliko hayo.                             MWISHO.