Habari

Jumatatu, 9 Februari 2026

HADI KUFIKA MIAKA 62 YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR ELIMU NI HAKI SIO UPENDELEO

Na ,Amina Ahmed Moh'd
 
Kabla ya Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964, elimu ya maandalizi Unguja na Pemba haikuwa rasmi wala jumuishi. Ilitolewa kwa upendeleo wa kijamii na kikabila, na iliwafikia wachache wa tabaka la juu  maeneo ya mijini pekee.
 Watoto wa maskini, wakulima na wavuvi walikosa fursa
 Hakukuwa na skuli za serikali za maandalizi
 Vijijini, watoto walitegemea  (Madrasa)   elimu ya dini pekee
Hakukuwa na utaratibu wa lishe, walimu walikuwa wachache na wengi wageni wasio kuwa wazawa 
 Mfumo wa elimu ya maandalizi  ulikuwa wa kikoloni na kisultani, elimu ikiwa si haki ya kila ZANZIBAR 
LAKINI  BAADA YA MAPINDUZI YA 1964 – MIAKA 62 BAADAYE (2026)
Mapinduzi yameleta mageuzi makubwa katika elimu ambapo 
 Elimu ndani ya miaka 62 ya Mapinduzi  kupitia serikali ya awamu ya nane  iliyo chini ya Dk Hussein Ali Mwinyi  imekuwa ni haki ya kila mtoto bila ubaguzi wa kidini, itikadi za siasa ,uchumi ,maumbile wala hali za maisha kama ilivyokuwa kabla ya Mapinduzi  yam waka 64 .
Huku Zaidi ya skuli  262 za maandalizi Unguja na Pemba ndani  ya miaka 62 ya Mapinduzi  
 Skuli 97 zimekarabatiwa, 36 mpya zinajengwa maeneo mbali mbali .
 Walimu wapya 889 wameajiriwa ndani ya miaka 62 mwaka  (2025/26)
  Wanafunzi wapatao  105,101 (82.5%) wameandikishwa  jambo ambalo awali kabala miaka 62 ya Mapinduzi halikuwepo 
  Wanafunzi 63,099 (50%) wanapata lishe  maskulini  kupitia ruzuku maalum ya serikali  
 ZANZIBAR  YA LEO  katika elimu ina mfumo jumuishi wa elimu, miundombinu bora, walimu wenye sifa na huduma za kijamii maskulini  ,lishe  na mazingira yaliorafiki  kwa wote 
________________________________________

Miaka 62 ya Mapinduzi ya Zanzibar  kupitia serikali ya awamu ya nane inayoongozwa na Dk Hussein Ali Mwinyi ni ushahidi kuwa: Elimu si upendeleo  bali  Elimu ni haki kwa watu wa aina zote kuanzia madarasa ya awali.
Mapinduzi yameifanya haki hii kufika kwa kila mtoto wa Zanzibar popote alipo  mjini na Vijijini 


  Maono ya kiongozi bora huonekana pale elimu inapokuwa haki ya kila mmoja  huku Taifa imara hujengwa na viongozi wanaothamini elimu bila ubaguzi kwani Uongozi bora huacha alama kupitia elimu jumuishi na yenye usawa kuanzia ngazi ya awali hadi vyuo vikuu .
  


 JEE WAJUWA Kabla ya Mapinduzi (1964)
• Elimu ya maandalizi haikuwa rasmi wala jumuishi.
• Iliwafikia wachache wa tabaka la juu mijini pekee.
• Watoto wa maskini, wakulima na wavuvi walikosa fursa.
• Hakukuwa na skuli za serikali za maandalizi.
• Vijijini, watoto walipata elimu ya dini kupitia madrasa pekee.
• Walimu wachache, wengi wakiwa wageni wasio wazawa.
• Mfumo ulikuwa wa kikoloni na kisultani, elimu si haki ya kila mtoto.
Baada ya Mapinduzi (1964–2026)
• Elimu imekuwa haki ya kila mtoto bila ubaguzi wa dini, siasa, au hali ya maisha.
• Skuli za maandalizi 262 zimeanzishwa Unguja na Pemba.
• Skuli 97 zimekarabatiwa na 36 mpya zinajengwa.
• Walimu wapya 889 wameajiriwa.
• Wanafunzi 105,101 (82.5%) wameandikishwa.
• Wanafunzi 63,099 (50%) hupata lishe shuleni kupitia ruzuku ya serikali.
• Mfumo wa elimu sasa ni jumuishi, wenye miundombinu bora, walimu wenye sifa, na mazingira rafiki.
Hitimisho
Mapinduzi ya Zanzibar yamebadilisha elimu kutoka upendeleo wa kikoloni hadi haki ya kila mtoto. Leo, elimu jumuishi na yenye usawa imejengwa kuanzia madarasa ya awali hadi vyuo vikuu, ikionesha maono ya uongozi bora unaothamini elimu kwa wote.

FREELANCER  
    AMINA AHMED MOH`D – ( BIYAYA)
    0776 -859 184
    minnah1202@gmail.com

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni