Habari

Jumatatu, 2 Juni 2025

ENEO LA EKA 10 LAKABIDHIWA KWA WAZIRI ADOLF MKENDA, NI KWA AJILI YA UJENZI WA SKULI YA UFUNDI KAMBINI-KOJANI

 

Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Adolf Mkenda amesema  ujenzi wa Skuli ya Ufundi itakayojengwa hivi karibuni  kambini kisiwani Pemba ni kuunga mkono serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika uimarishaji maendeleo ya elimu inayoendelea kuimarishwa  kwa kiwango kibwa na serikali ya amwanu ya Nan echini ya Rais Dr. Hussein Ali Mwinyi

Prefesa Mkenda ameyasema hayo wakati akizungumza na wananchi wa jimbo la Kojani katika hafla la makabidhiano ya eneo la ujenzi wa Skuli ya Ufundi Kambini Kichokochwe lililokabidhiwa na mbunge wa jimbo hilo Hamad Hassan Chande  itakayoanza kujengwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teklojia ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ambapo jumla ya ekari kumi zimekazibiwa kwa ajili ya ujenzi wa chuo hicho .

Aidha Pro, Mkenda amesema Wizara yake itaendelea kufanyakazi kwa pamoja na Wiara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar ili kuona sekta ya elimu inaendelea kuimarika visiwani.

Amesema Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia inatambua juhudi kubwa zinazofanywa na serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika sekta ya elimu ikiwemo ujenzi wa kujenga Skuli za ghorofa kila katika maeneo mbali mbali ili kurahisisha watoto kusoma kwa utulivu.

Aidha amesema kuwa Wizara yake imekuwa ikishirikiana bega kwa bega na Wizara ya Elimu na Mfunzo ya Amali Zanzibar, lengo ikiwa ni kuona suala la maendeleo ya elimu linawanufaisha wananchi wa pande zote mbili.

Akimkaribisha Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia kuzungumza na wananchi, Mbunge wa Jimbo la Kojani ambaye ni Naibu Waziri wa Fedha wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hamad Hassan Chande.



Amesema ujenzi wa kituo hicho utaleta manufaa makubwa kwa vijhana wa jimbo la Kojani na wengine wengi wanaotoka maeneo tofauti ya kisiwani Pemba.

Aliwataka wananchi wa jimbo la Kojani kuendelea kuiunga mkono Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan na ya Zanzibar inayoongozwa na Rais Dkt. Hussein Ali Mwinyi kwa juhudi kubwa wanazochukua kuwafikishia wananchi huduma mbali mbali za maendeleo.

Aidha Chande aliongeza kwa kusema kuwa ujenzi wa Skuli hiyo ya Ufundi ambayo itakuwa ya kwanza kwa Mkoa wa Kaskazini Pemba itafungua zaidi milango ya elimu kwa vijana wa jimbo la  Kojani na Pemba kwa ujumla.

Afisa Mdhamini wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Pemba Moh`d Nassor Salim ameahidi kuwa Wiraya ya Elimu Zanzibar itakuwa karibu kutoa ushikiano wa Skuli hiyo.

Amesema Wizara ya Elimu ya Zanzibar imekuwa ikishirikiana kwa karibu na Wizara ya Elimu, Sayansi na Tekbolojia katika masuala tofauti ya kielimu ikiwemo bodi za mikopo ya elimu ya juu.

Nao kwa upande wao baadhi ya wazee wa Shehia ya Kambini wamesema ujenzi wa mradi huo wa Skuli ya Ufundi wameupokea kwa mikono miwili na watatoa ushirikiano kwa wajenzi.

Mzee Hamad Khamis Kombo wa Kambini ameishukuru Serikali kwa hatua ya ujenzi wa kituo hicho katika Shehia ya Kambini kwa kusema kuwa pamoja kuwa na vijana wengine wa jimbo la kojani watasoma kwenye skuli hiyo lakini wao ndio wanufaika wakubwa.



Naye Bakari Ali Hassan wa kijiji cha Kangagani amesema suala la kujengwa skuli ya ufundi kitatoa fursa mbali mbali kwa wenyeji wa jimbo la kojani hasa kambini.

 Rauhiya Khatib Juma ni kijana wa Shehia ya Kambini amesema skuli hiyo ya ufundi itasaidia kwa kiasi kikubwa kwa vijana wa mikoa miwili ya Kusini na Kaskazini Pemba na kumshukuru ubunge wa jimbo la Kojani Hamad Hassan Chande kwa juhudi zake zilizopelekea kujengwa kwa kituo hicho.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni