Habari

Jumanne, 3 Februari 2026

MAENDELEO YA YA ELIMU YA MAANDALIZI NDANI YA MIAKA 62 YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR YAKUPIGIWA MFANO,,NEEMA KWA WOTE BILA UBAGUZI

 AMINA AHMED  MOHD

  JEE !  WAJUWA KABLA      Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964, elimu ya maandalizi  ndani ya visiwa vya unguja na Pemba  haikuwa rasmi, na nathubutu kusema haikuwepo kabisa ! hukukatika maeneo iliyokuwepo  ilitolewa kwa upendeleo wa kijamii na kikabila, na watoto wengi wa tabaka la chini watoto wa mskini, wakwezi na wakulima  hawakupata nafasi ya kujiunga na skuli za maandalizi ,huku Elimu ikibaki kuwa ya kikundi kidogo cha watotokutoka familia za wenye uwezo  na si haki ya kila mtoto.Yote hayo sababu kubwa ilikuwa Mfumo wa elimu ulikuwa ni wa kikoloni na wakisultani, ukilenga zaidi watoto wa tabaka la juu mijini, huku vijijini kukikosekana kabisa huduma za elimu ya awali ambayo kwa sasa inatambulika kama elimu ya maandalizi .HISTORIA YA ELIMU YA MAANDALIZI ZANZIBAR KABLA YA MAPINDUZI  YA ZANZIBAR YA MWAKA 64  UPATIKANAJI WA ELIMUElimu ya maandalizi haikuwa sehemu ya sera ya serikali ya kisultani. Hakukuwa na mtandao wa  skuli  za serikali kwa watoto wote; badala yake  skuli nyingi zilikuwa za binafsi na nyentine zikiwa  kidini.Elimu ya awali haikujulikana kwa kiwango cha kitaifa, bali ilikuwa ni ya kikundi kidogo cha watu wenye uwezo na maeneo yaliyokuwa rafiki kufikika maeneo ya unguja mjiniWatoto wachache wa tabaka la juu, hasa wa asili ya Kiarabu na kiswahili wa mjini, ndio waliopata nafasi ya kujiunga na skuli za awali,huku Vijijini, watoto walitegemea madrasa na elimu ya dini kama njia pekee ya skuli za maandaliz katika kujifunza .Mfumo wa elimu ulikuwa wa kikoloni na kisultani, ukilenga zaidi watoto wa tabaka la juu.Skuli  chache zilikuwepo, nyingi zikiwa mijini na hazikuwafikia watoto wa vijijini.Elimu ya maandalizi haikuwa rasmi, watoto wengi walijifunza kupitia madrasa au elimu ya jadi.Uwiano wa walimu kwa wanafunzi ulikuwa duni, walimu wachache na wengi wakiwa wageni.Huduma za kijamii skulini  hazikuwepo, hakuna lishe shuleni wala ruzuku kwa wanafunzi.Uandikishaji ulikuwa mdogo sana, idadi kubwa ya watoto wa Zanzibar hawakupata nafasi ya kusoma elimu ya maandalizi . Walimu wachache walikuwepo, wengi wakiwa wageni au wa tabaka la juu.Idadi ya watoto waliopata elimu ya maandalizi ilikuwa ndogo sana, ikilinganishwa na idadi ya watoto wa Zanzibar.Hakukuwa na mafunzo maalum ya ualimu wa maandalizi; walimu walitegemea uzoefu wa madrasa au elimu ya msingi ya kikoloniELIMU BAADA YA MAPINDUZI  1964–  ILIPOFIKIA MIAKA 62   MWAKA HUU 2026)Kuna mageuzi makubwa  mabadiliko na maendeleo ya elimu  yamefikiwa  miongoni mwa hayo ni pamoja na Elimu sasakuwa  haki ya kila mtoto,kwa lazima  bila ubaguzi wa kijamii,dini siasa wala  uchumi . Kabla ya Mapinduzi ya mwaka 1964, elimu ya maandalizi Zanzibar haikuwa rasmi, haikuwa jumuishi, na iliwafikia wachache tu wa tabaka la juu mijini. Mapinduzi ya Zanzibar yalibadilisha hali hii kwa kuifanya elimu kuwa haki ya kila mtoto bila ubaguzi, na kuanzisha mtandao wa shule za maandalizi na msingi unaofadhiliwa na serikali. Skuli zimeongezeka kwa kasi ndani ya miaka 62 ya Mapinduzi  ya mwaka 1964  Kwa sasa kuna zaidi ya 262 za maandalizi  zinazopata ruzuku ya Serikalikatka kutoa huduma bora kwa wananchi za serikali na binafsi ..Ndani ya miaka 62 ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar kuna Ukarabati na ujenzi mpya: Skuli 97 za maandalizi zinazojumuisha na a msingi zinaendelea kukarabatiwa, na ujenzi wa shule mpya 36 (21 za maandalizi, 15 za msingi)ukiendelea katika maeneo mbali mbali Unguja na Pemba.Ongezeko la Walimu wapya,889 wamepangiwa kazi  mwaka 2025/26  pekee, wakisaidia kupunguza uwiano wa walimu kwa wanafunzi jambo ambalo kabla ya miaka 62 ya mapinduzi ya  ya 1964 hayakuwepo .Kuna ongezeko la Uandikishaji wa Wanafunzi , Wanafunzi 105,101 sawa na asilimia  (82.5%) wameandikishwa katika skuli  maandalizi maeneo yote  Unguja na Pemba hadi kufikia miaka 62 ya mapinduzi matukufu ya Zanzibar yalioasisiwa na  Hayat mzee Abeid Aman Karume .Ambapo huduma  za lishe Maskulini kabla ya miaka  ya Miaka 62 ya Mapinduzi ya Mwaka 1964 hazikuwepo kabisa lakini kwa  ndani ya miaka 62 ya Mapinduzi hayo Matukufu   huduma za lishe zimeongezeka na kufikia asilimia  50  na wanafunzi    wapatao 63,099 .hupata lishe bora kupitia ruzuku ya serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.  Sekta ya elimu ya maandalizi na msingi Zanzibar imepiga hatua kubwa baada ya Mapinduzi ya mwaka 1964, ikilinganishwa na hali ya elimu kabla ya Mapinduzi. Leo, miaka 62 ya Mapinduzi hayo  hku idadi ya mageuzi na mabadiliko katika upatikanaji wa Haki hiyo  zikionesha  kuongezeka kupatikana huduma  bora za elimu ya maandalizi  kwa uandikashaji wa wanafunzi bila ubaguzi wa aina yeyote, Lishe, elimu bora, waalimu , majengo  bora ya kupata elimu Mapinduzi yam waka 1964 hadi kufika kilele cha miaka 62 mwaka huu 2026 january 12  kumekuwa na mageuzi makubwa katika elimu ya maandalizi na msingi kutoka mfumo wa kikiloni uliokuwa wa kibaguzi na wenye  upatikanaji mdogo wa utoaji elimu  ufinyu wa maeneo ,lishe ,uwandikishaji duni na matabaka wa waalimu wachache mitaala isyorasmi hadi sasa  kuwa kasi ya mageuzi  kutoka kadhia hizo na kuwa  Zanzibar ya miaka 62 ya mapinduzi yenye  mfumo mjumuishi wa elimu ,takwimu thabiti za uandikishaji zenye kuangalia hali za wananchi,waalimu  bora, miundombinu bora  huduma za kijamii  skulini   yote hayo ni mafanikio  ya miaka 62 y MapinduizI ya Zanzibar   katika kuinua maisha ya wananchi kupitia elimu bora ambayo ndio ufunguo wa mafanikio ya taifa na mtu mmoja mmoja baadae

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni